Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Salum Kalli (kulia) akitoa salamu za rambirambi akiwa pamoja na maktibu wa CCM wa wilaya za Sengerema, Kwimba, Nyamagana, Misungwi, Ilemela, Magu na Ukerewe kabla ya kutoa heshima za mwisho.
Katibu wa wazazi Kwimba Chuki Anthony akitoa heshima za mwisho kwenye jeneza la mwili wa aliyekuwa Katibu wa UWT Wilaya ya Sengerema jana.


Wazazi na watoto wa marehemu Diana Musa, wakiwa kwenye ibada ya maziko iliyofanyika nyumbani kwao na marehemu mtaa wa Ngudu Kwimba jana.
Mwinjilisti wa Kanisa la AICT Reuben Daud akiendesha ibada ya mazishi ya aliyekuwa Katibu wa UWT Wilaya ya Sengerema, marehemu Diana Musa aliyefariki Agosti 6, mwaka huu kwa maradhi ya TB na Kisukari.
Watumishi wa CCM Wilaya ya Sengerema wakiwa pembeni mwa jeneza la aliyekuwa Katibu wa UWT wilayani humo kabla ya kutoa heshima za mwisho.
Baba mzazi wa marehemu Diana Musa, Seleman Bulugu akisaidiwa baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa mwanaye jana.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Salum Kalli akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Diana Musa ambaye alikuwa Katibu wa UWT Wilaya ya Sengerema.Kalli alimwakilisha Katibu Mkuu wa CCM. Dk. Bashiru Ally, kwenye maziko ya katibu huyo yaliyofanyika kwenye makaburi ya AICT mjini Ngudu Kwimba.
Vijana wa Green Guard wa CCM wakiwa wamebeba jeneza la mwili wa marehemu Diana Musa tayari kuelekea makaburini jana.

Vijana wa Green Guard wa CCM wakishusha jeneza la mwili wa marehemu Diana Musa kwa ajili ya mazishi.
Mtoto wa kike wa marehemu Diana Musa,akitupia udongo kwenye jeneza na mama yake jana wakati wa mazishi yaliyofanyika mjini Ngudu Kwimba kwenye makaburi ya AICT.
Mzee Selemani Bulugu na mkewe Naomi ngw’ashi Kadoke wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mtoto wao, Marehemu Diana Musa, ambaye alizikwa kwenye makaburi ya AICT mjini Ngudu Kwimba jana.
Watoto wa marehemu Diana wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mama yao jana baada ya mazishi.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: