JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam  limesema kuanzia kesho Jumatano litaimarisha ulinzi kwa kutumia vikosi vyote vya doria ikiwemo mbwa, farasi na helicopter ili kuhakikisha mkutano wa 39 Jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika (SADC), unamalizika salama.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Agosti 13, 2019 jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa amesema doria hiyo ni sehemu ya maandalizi ya kuwapokea wakuu wa nchi 16 ambao wote wamedhibitisha kuhudhuria mkutano huo.

"Tuliweka zuio la baadhi ya vyombo vya moto kutoingia katikati ya mji katika kipindi hiki cha mikutano ya SADC ,  kuna baadhi wamekiuka hasa pikipiki (bodaboda) ambazo zimekuwa hazifuati sheria, wanabeba mishikikaki, hawavai kofia ngumu na kupitia msako uliofanywa na jeshi la polisi vyombo vya moto 126 vimekamatwa na hivyo vikihusisha pikipiki 87, bajaji 13 na magari yenye ving'ora na taa sumbufu barabarani 26 na baadhi ya wahusika wanashikiliwa na watapelekwa mahakamani" amesema  Mambosasa. 

Aidha Mambosasa amesema baadhi ya barabara katikati ya jiji la Dar es Salaam zitafungwa na kwamba barabara hizi zitatangazwa baadaye.


Pia amewahakikishia wananchi na wageni usalama wa hali ya juu na bado wanaendelea na kazi ya kuhakikisha jiji hilo linaendelea kubaki salama salimini hata baada ya mkutano huo kumalizika
Share To:

msumbanews

Post A Comment: