Mshtakiwa anayekabiliwa na kesi ya kumuua na kumchoma moto mkewe Naomi Marijani, Hamis Said, ametoa tishio kwa waandishi wa habari wanaompiga picha anapowasili mahakamani ambapo amesema akimkamata mmoja wao atamfanya kitu kibaya ambacho mahakama haitakitarajia. 

Mfanyabiashara huyo ambaye yupo gerezani kwa siku 14 tangu alipofikishwa mahakamani hapo Julai 30, 2019 ameyaeleza hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Salum Ally.

“Mheshimwa Hakimu tangu nimefika hapa naona waandishi wa habari wamekazana kunipiga picha sana, yaani mpaka nimeingia humu ndani bado wananipiga picha tu bila kujua kwenye akili yangu nawaza nini, unajua mimi kwa sasa kichwa changu kimechanganyikiwa sana, hata hii kesi yenyewe sielewi itakuwaje.

“Nimekaa nitulize akili yangu halafu na wao wananisogelea sogelea kunipiga picha mwisho wanisababishe nifanye jambo ambalo si la kawaida, kwa sababu wanakuja hadi kunivua kofia jambo ambalo si japenda, wamekuwa wakinipiga picha kuanzia chini hadi ndani ya Mahakama, sasa nitakuja  kuwafanyia kitu kibaya hadi mahakama itashangaa,” amesema

 Baada ya maelezo  hayo Wakili wa serikali Wankyo Simon alisimama na kujibu kwamba Waandishi wanafanya kazi yao hivyo awape uhuru kwani wanazingatia sheria ya taaluma zao.

” Unajua Mahakama zote hapa nchini zinakuwa na waandishi wa habari wanapiga picha na kutekeleza majukumu yao, hivyo naomba uwape uhuru wao, lakini kwa hilo ulilosema kwamba wamekuja mpaka kukufunua kofia ili wakupige picha sio kweli tena siamini kama wanaweza wakafanya hivyo.

“Kwa sababu wakati wanakupiga picha nilikuwepo na niliona tukio zima hawajakufunua kofia ila walikuwa wanakusogelea Karibu ili wapate uso wako kwakuwa ulikuwa umejifunika na kofia,” alisema Wankyo. 

Hakimu Ally ameahirisha kesi hiyo hadi Agosti 27, 2019 kwa ajili ya kutajwa

Mshitakiwa anakabiliwa na kosa la mauaji ambapo adaiwa alilitenda Mei 15, 2019 katika oneo la Geza Ulole Kigamboni Dar es Salaam ambapo alimuua mtu anayeitwa Naomi Marajani.

Hamis anadaiwa kumuua mke wake Naomi kisha kumchoma moto kwa kutumia magunia mawili ya Mkaa ambapo alichukua majivu ya marehemu na kwenda kuyafukia shambani kwake.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: