Umati wa watu uliojitokeza katika Ibada ya kuadhimisha miaka 80 ya Kanisa la TAG Tanzania iliyofanyika kitaifa Jijini Arusha katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid Karume Jijini Arusha ambapo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kasimu Majaliwa.
 Maandamano ya maandhimishonya mika 80 ya Kanisa la TAG na miaka 10 ya mpango mkakati wa mavuno 2009-2019 
 Maandamano yakiingia uwanjani kwaajili ya sherehe ya maadhimisho ya miaka 80 ya Kanisa la Tanzania Asaemblies of God nchini Tanzania.
 Maandamano yakiingia uwanja wa Shekh Amri Abeid Karume.
Wamishionari wa ww kanisa la TAG wakiwa katika maadhimisho ya miaka 80 ya Kanisa hilo .
Baadhibyavwachungaji wakiwa katika ibada ya kuadhimisha miaka 80 ya kanisa la TAG iliyofanyika kitaifa Jijini Arusha.
Baadhi ya wachungaji wakimuomba Mungu katika maadhimisho ya miaka 80 ya kanisa la TAG leo Jijini Arusha.
Vijana wa CAS kama wanavyoonekana katika picha wakicheza kwa furaha katika maadhimisho ya miaka 80 ya kanisa lao la TAG yaliyofanyika kitaifa Jijini.Arusha.
Umati wa watu waliojitokeza katika maadhimisho ya miaka 80 ya kanisa la TAG tangia kuanzishwa kwake mwaka.1939 mkoani Mbeya.
Baadhi ya wamishionari wa Kanisa la TAG wakiwa katika maadhimisho ya miaka 80 ya kanisa hilo yaliyofanyika Jijini Arusha katika uwanja wa makumbusho ya Sheikh Amri Abeid Karume leo.
Mass Preise Team wakiwa wanaimba katika maadhimisho ya miaka 80 ya kanisa la TAG na Mpango utekelezaji wa mkakati wa mika 10 ya mavuno.

Na.Vero Ignatus,Arusha.

Maadhimisho ya miaka 80 ya TAG na miaka 10 ya mpango mkakati wa mavuno 2009-2019 yamefanyika  jijii Arusha na kuhuduhriwa na viongozi mbalimbali wa dini na waumini wa kanisa hilo.

Dkt.Barnabas Mtokambaki ni Askofu mkuu wa Kanisa la TAG nchini Tanzania ambapo pia ni Rais wa kanisa hilo Afrika, Maadhimisho hayo Askofu mkuu wa amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Tanzania kwa kulipenda Kanisa hilo na kuwajali.

Mpango mkakati wa awamu ya kwanza ya mafanikio ya kanisa la TAG kwa mujibu wa Dkt.Mtokambali wameyapata katika miaka 10 ya mavuno kwani majimbo yameongezeka kutoka 10-69,makanisa 2,619-9,986,wachungaji 2,616-10,085,washirika kuongezeka 200,069-13,326,vyuo vya Biblia 4-8 ambapo Idara ya kujenga shule za sekondari na nyingine zitaanza kuandikisha wanafunzi mwezi Januari 2020.

Ameeleza changamoto kubwa waliyonayo ni eneo la kujenga ofisi kwani makao makuu ya kanisa hilo yaliyopoubungoba limekuwa na nafasi ni ndogo ukilinganisha na wingi wa idadi ya waumini waliopo hivyo wamemuomba Dkt.Magufuli kuwatazama upya na kuwapa eneo kwaajili ya ujenzi sambamba na kuondolewa kodi ya vifaa ambavyo vipo bandarini.

Vile vile Dkt.Mtokambali ameweza kukabidhi mifuko 1000 ya saruji kwa mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kwaajili ya kumalizia ujenzi katika shule zilizopo mkoani huko ambapo awali alishawahi kutoa mifuko mingine 5000 ya saruji.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ni Rais wa Jamuhuri ya Tanzania ambapo amewakilishwa na waziri mkuu Kasimu Majaliwa ambapo amesema kuwa serikali imedhamiria kuwatumikia watanzania wote bila kujali dini wala siasa.

Amesemaserikalivya awamu ya tano itaendekea kudumisha umoja na ushirikiano na Taasisi za kidini  Mungu katika utekelezaji wa majukumu yake yote wakati wanasheherehekea mpango mkakati wa mavuni ni vyema wakakumbuka mchango wa waanzilishi wote wa Kanisa hilo na kuwapongeza kwa kazi nzuri waliyoifanya hadi kufikia,walipo sasa.

Mhe.Waziri Mkuu amewataka viongozi hao kuendelea kuendelea kuimarisha kitengo chao cha kuinua miradi itakayowafaidisha na kuwainua kiuchumi.

Akijibu ombi la lililoletwa na Askofu mkuu wa Kanisa la TAG Dkt.Barnabas Mtokambali kuhusu eneo la kanisa  lililopo Ubungo kitalu namba 434 G unamilikiwa na TTCL,Waziri Mkuu amesema ombi hilo limepokelewa na atalifanyia kazi.

Vile vile Mhe. Waziri Mkuu alitolea ufafanuzi kuhusiana na msamaha wa kodi kwa vifaaa na kusema kuna baadhi ya Taasisi za kidini zilitumia vibaya msamaha huo wa kodi ndiyo walisababisha eneo hilo kuwekewa sheria ila ameahidi swala hilo atalifikisha kwa Mhe.Rais wa Tanzania Dkt.Magufuli.

Serikali inaendelea kusimamia swala la Amani na utulivu sambamba na kudhibiti matukio yote yanayovunja Amani ambapo
serikali inawategemea sana viongozi wa dini. 

"Endeleeni kuliombea taifa na viongozi wake ili kuliombea taifa na viongozi wake mnajua fika kuwa Mhe.Rais anahitaji kuombewa sana na nyie viongozi wa dini" ili aweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi"alisema Waziri Mkuu.

Amehitimisha kwa kusema kuwa Seririkali inaendekea kuliongoza taifa la Tanzania kwa kufuata miongozo mbalimbali kama Katiba na sheria katika katika kila nyanja na kwa maslalahi ya Taifa.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema Viongozi wa dini kichocheo cha usalama na Amani katika mkoa wa Arusha .



"Hata mimi nilipoteuliwa kuwa kiongozi mahali pa kwanza nilipokwenda kuripoti ni kwa viongozi wa dini na kuwaambia mimi ni kijana wenu naomva ushirikiano wenu na popote nitakapotetereka mnirekebishe"


Kanisa hilo la TAG  lilianza kazi nchini mwaka 1939, Igale Mbeya,Askofu wa kwanza akiwa Emmanuel Lazaro,Mwanisongile,na awamu ya tatu Dkt.Barnabas Mtokambali, ambapo hivi sasa yapo makanisa 9,986, vyuo vya Biblia 8 vyuo vya kupanda makanisa ,shule za sekondari,vyuo vya ualimu ambavyo vinakaribia kukamilika,vituo vya Radio,vyuo vya ualimu,vituo vya Afya na vituo vya huduma za jamii kwa watoto yatima.





Share To:

Vukatz Blog

Post A Comment: