Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega watatu kulia ,
Naibu Waziri wa Kilimo maliasili na Usalama wa Chakula Bi Marjolyn kutoka nchini Uholanziwa tatu kushoto ,pamoja na
Dkt Edmond Matafu wa kwanza kulia pamoja na viongozi wengine wakikata utepe ikiwa ni ishara ya maabara hiyo ya kutembea imezinduliwa rasmi.
Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega pamoja na
Naibu Waziri wa
Kilimo maliasili na Usalama wa Chakula Bi Marjolyn kutoka nchini
Uholanzi wakikata utepe ishara ya kufungua rasmi maabara za utupimaji wa
udongo
Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akipeana mkono na
Dkt Edmond Matafu
ambaye ni moja wa wawekezaji walioleta maabara hiyo ambayo itaidia sana
wakulima kwani watakuwa wanapima udongo huo kabla ya kulima .
Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akiongea jambo mara baada ya kuzindua maabara hiyo ya upimaji wa udongo.
Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha
Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi
Abdallah
Ulega amezindua Maabara ya kutembea ya kufanya
utafiti wa kupima ubora wa udongo kwa wakulima ili kupata uhakika wa
kuwa na mazao mengi yenye ubora kwa kutumia teknolojia hiyo mpya ya
upimaji wa Udongo iliyoletwa kutoka nchini Uholanzi na Mtanzania
Dkt.Edmund Matafu Makazi wa jijini Arusha.
Amesema
kuwa Teknolojia hiyo ambayo ni yakwanza hapa nchini, itakuwa mkombozi
kwa mkulima na kuongeza mapato na uzalishaji kwa kujua jiografia,eneo na
udongo,kwani thamani ya malipo ya upimaji huo ni rafiki kwa wakulima
kuchangamkia fursa ya upimaji.
Kwa
upande wake ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya live support systerms
limited inayojishuhulisha na shuhuli ya upimaji wa udongo pmoja na
utengenezaji wa Mbolea Tanzania Dkt Edmond Matafu alisema maabara hiyo
itawasaidia kubaini
virutubisho na muundo wa udongo wa eneo husika ,hivyo kumwezesha mkulima
kujua mazao gani yanayostahili kulimwa katika eneo husika na kuepuka
kilimo cha kubahatisha ambacho kimekuwa kikiwaletea hasara wakulima
walio wengi nchini.
‘’Maabara
hii tulianza kuitumia nchini Kenya na sasa imeingia nchini na imekuwa
na manufaa makubwa kwa wakulima kuweza kubaini mapungufu katika udongo
na jinsi ya mahitaji ya mbolea’’.Alisema dkt Matafu
Alibainisha
kuwa kabla ya kuzindua maabara hii watanzania walikuwa wanakosa huduma
hii kwa hapa nchini kwani walikuwa wanalazimika kwenda hadi nje ya nchi
ikiwemo Kenya kupima udongo huo
Alisema
kuwa huduma hii itamnufaisha mkulima kutokana na kupata mazao mengi
mara baada ya kupima udongo ambao anataka kulima na baadae kupewa
ushauri ni mbolea gani itakayomsaidia kumpa mavuno mengi,na pia
itamsaidia kupunguza upotevu wa fedha kwani atakuwa analima sehemu
ambayo kaipima pia atakuwa amepewa anunue mbolea gani itakayo msaidia.
Post A Comment: