NA HERI SHAABAN

MKURUGENZI wa Kampuni ya Udalali Yono Action Mart Scholastika Kevela amewataka Wanawake wa Wilaya ya Ilala kujitambua ili waweze kuwa wajasiriamali wazuri.

Kevela aliyasema hayo kata ya Tabata Manispaa ya Ilala      wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi .

" Nawapongeza Wanawake wa Tabata kwa uzinduzi wa Jukwaa lenu naomba Wanawake wa Wilaya ya Ilala wote kujitambua  ili muweze kujikwamua kiuchumi muachane na maisha tegemezi "alisema Kevela.

Kevela aliwataka Wanawake kuwamka kwani Mwanamke ndio Waziri  Mkuu  anaongoza nyumba anayo mamlaka yote ndani ya  familia .

Alitumia nafasi hiyo Kumpongeza Serikali ya awamu ya tano ya Rais John Magufuli ya Tanzania ya Viwanda ambayo imesaidia kwa asilimia 100 kusaidia vikundi mbalimbali kuviwezesha mikopo ya asilimia 10 ambayo inatolewa ngazi ya halmashauri.

Alisema Jukwaa ni sehemu ya fursa halina ubaguzi ,aliwataka Wanawake kushikama na kuwa wamoja  rafiki wa Mwanamke ni mwanamke mwenzake.

Kwa upande wake Mratibu wa Dawati la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Wilaya ya Ilala Georgis Asenga, alitoa elimu ya jukwaa na maana yake.


Pia  Asenga alivitaka vikundi vikamilishe taratibu za usajili ili viweze kupewa mikopo  ngazi ya halmashauri.
 
Alisema mpaka sasa katika manispaa ya Ilala  jumla majukwaa 11 yamefanikiwa kuzinduliwa bado kata 25 zipo katika taratibu za uzinduzi wake.

Naye Makamu  Mwenyekiti wa Jukwaa Wilaya ya Ilala Sauda Addey amewataka Wanawake kushirikiana kwa pamoja  katika shughuli zao za kiuchumi waanzishe viwanda vidogo vidogo katika wilaya ya Ilala .

Sauda alisema  imefika sasa  wakati  Wanawake kujishughulisha wainuke kiuchumi, wasiweke chuki katika vikundi wawe wamoja  waheshimu viongozi waliochaguliwa  kwa ajili ya kuwaongoza.

Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Kata ya Tabata Agines Minzi alisema  Kata ya Tabata ina vikundi 294,vilivyosajiliwa 182 ,vilivyopewa mikopo 22 ,vikundi 76 vinatarajia kupata mikopo  vya Wanawake 51,vijana 25 vya Walemavu 10.

Agines alisema vikundi vilivyokuwa katika mchakato vipo kumi  vishatuma maombi   Wanawake 30 vijana 20 walemavu watano.

MWISHO
Share To:

msumbanews

Post A Comment: