Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Tanesco mkoa wa Arusha imefanya Operesheni Maalumu ya kukagua mita zaidi ya 1000  na kubaini  baadhi ya watu waliochakachua mita za umeme ikiwa ni njia ya kukwepa kulipa malipo stahiki ya huduma za umeme hivyo wamechukuliwa hatua za kisheria.

Afisa Ukaguzi wa Mita  Zuberi Hassan amesema kuwa baada ya kufanya ukaguzi huo wamebaini mita kadhaa ambazo zimechezewa ili zisiweze kusoma vizuri matumizi ya umeme jambo ambalo ni hujuma kwa shirika hilo.

Mmiliki wa eneo ambalo lilikaguliwa na kukutwa na tatizo la mita kuchakachuliwa ,Joseph Shirima   amesema kuwa tatizo hilo lilisababishwa na baadhi ya wapangaji wasio waaminifu kufunga mita zao hivyo atashirikiana na shirika hilo ili kuhakikisha mita zinazowekwa zina kuwa na usahihi.

Meneja wa wateja wakubwa Tanesco  Mhandisi Frederick Njavike  amesema kuwa shirika hilo limefanya ukaguzi wa mita zaidi ya 1000  katika maeneo mengi jijini Arusha ili kujiridhisha na mita zilizopo pamoja na kuchukua hatua stahiki ikiwemo kusitisha huduma za umeme pamoja na kuchukua hatua Kali za kisheria ili iwe fundisho kwa wateja wenye tabia ya kuchezea mita

Share To:

Post A Comment: