Na EZEKIEL NASHON, DODOMA.

SERIKALI Waziri  wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI, Seleman Jafo, amewataka wakurugenzi kote nchini kuhakikisha wanasimamia kikamilifu miradi inayotekelezwa katika halmashauri zao  ili iweze kuleta matokeo chanya.
Ameyasema hayo  Jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo ya wakurugenzi yaliyoandaliwa na chuo cha serikali  za mitaa Hombolo yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kuandika maandiko ya miradi ya kimkakati katika halmashauri zao.
Amesema lazima wakurugenzi wahakikishe wanasimamia kikamilifu miradi hiyo kwani nia ya serikali kutekeleza miradi hiyo ni kuhakikisha miradi hiyo inawanufaisha wananchi katika maeneo husika ni lazima isimamiwe na kutekelezwa kwa viwango.
“Serikali inawekeza fedha nyingi sana katika miradi hii ni wajibu wenu sasa kuhakikisha mnaisimamia kikamilifu lengo la serikali kuhakikisha wananchi wananufaika na miradi hii, simamieni kikamilifu” amesema.
Aidha amesikitishwa na kitendo cha baadhi  ya mikoa kama Dodoma na Njombe kushindwa  kufika katika kikao hicho na baadhi ya mikoa kama Mtwara,Lindi kuleta wakurugenzi wachache ukilinganisha na halmashauri zilizopo katika mikoa hiyo.
Amesema mafunzo hayo yanaumuhimu mkubwa kwa wakurugenzi kuwajengea uwezo wa kuwawezesha katika kuandika maandiko ya kimkakati lakini wanapuuzia mafunzo hayo.
“kuna wakurugenzi siwaoni hapa kama wa Dodoma au kwavile wanakusanya mapato kuliko wengine na kujiona? Ukiangalia mkoa wa Dodoma kuna mradi  mmoja tu kule Kondoa, hii mingine ni ya serikali kuu, ukiangalia Njombe hawana mradi hata mmoja lakini hawapo” amesema.
Ameagiza kuandaliwa kwa kikao kingine ndani ya mwezi mmoja na  kuwaagiza wawezeshaji wa kikao hicho kuwapa taarifa wakurugenzi  mapema ili waweze kuhudhuria kikaohicho kwani kinaumuhimu sana kwa wakurugenzi na kuagiza kila halmashauri kuhudhuria.
Pia amewataka wawezeshaji wa kikao hicho kujenga utaratibu wa kuwatembeza wajumbe wa vikao hivyo  katika miradi inayotekelezwa ili waweze kujifunza na wao wakatekeleze katika maeneo yao.
Kwa upande wake kaimu mkuu wa chuo cha serikali za mitaa Hombolo, Michael Msendekwa amesema lengo la kuandaa kikao hicho ni kuwajengea utaratibu na uwezo wa kuandika maandiko ya miradi kwani kwa utafiti wao waligundua kuna shida katika  uandishi wa miradi.

“Tumeandaa mafunzo haya kwa sababu kwa utafiti tuliofanya tumegundua kunashida katika uandishi wa maandiko kwa wakurugenzi wetu  tukaona ni mda mwafaka kwa kuwajengea uwezo” amesema.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: