Mkuu
wa Mkoa wa Dodoma Dr.Binilith Mahenge akizungumza
MBUNGE wa Jimbo la Dodoma (CCM) na Naibu Waziri Ofisi Ya Waziri Mkuu Kazi Vijana na Ajira akizungumza
MKUU wa wilaya ya Dodoma Patrobas Katambi akizungumza
MKURUGENZI wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi akizungumza
MBUNGE wa Jimbo la Dodoma (CCM) na Naibu Waziri Ofisi Ya Waziri Mkuu Kazi Vijana na Ajira akizungumza
MKUU wa wilaya ya Dodoma Patrobas Katambi akizungumza
MKURUGENZI wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi akizungumza
Mkuu
wa Mkoa wa Dodoma Dr.Binilith Mahenge ameongoza jopo la Viongozi wa
Wilaya ya Dodoma Mjini kwenye ziara maalum katika ngazi za mitaa
kusikiliza kero zinazowakabili wananchi wa Jiji la Dodoma na kuzipatia
ufumbuzi kero hizo.
RC Mahenge ameanza ziara hiyo jana katika kata za Ipagala
na Nzuguni na kuendelea na ziara leo katika kata za Mpunguzi na Mbabala
ambapo amesikiliza kero kubwa za wananchi katika maeneo ya ni Migogoro ya
Ardhi,Maji,Umeme, Miundombinu na Masuala ya Afya.
“Kila kiongozi katika eneo lake ahakikishe anakuwa mstari
wa mbele katika kusikiliza kero na kutafuta majawabu wa kero hizi za
wananchi,si jambo jema kupuuza kero hizi kwasababu sisi tumepewa dhamana
na heshima ya kuwahudumia wananchi hawa hivyo basi tumsaidie kwa
vitendo Mh Rais Magufuli katika kuhudumia Watanzania”Alisema RC
Dr.Mahenge.
Katika ziara hiyo RC Dr.Mahenge ameambatana na Mkuu wa
Wilaya ya Dodoma Mjini Mh.Patrobas Katambi,Mbunge wa Jimbo la Dodoma
Mjini Mh Anthony Mavunde,Mkurugenzi wa Jiji Ndg Godwin Kunambi na
wataalamu kutoka TARURA,TANESCO, TANROADS,SUMATRA na DUWASA.
Aidha Wananchi wa Jiji la Dodoma wamepongeza hatua hiyo ya
Viongozi kusikiliza kero za wananchi kwa ukaribu na kuzipatia majibu
hali ambayo itapunguza malalamiko mengi waliyonayo wananchi.
Post A Comment: