Na Woinde Shizza ,Arusha
Mawaziri
wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki(EALA) wamekwamisha mjadala wa
bunge la bajeti la afrika mashariki baada ha kuto kuwepo katika kikao
cha bunge hilo cha kujadili bajeti hiyo ya mwaka 2019/2020
Mawaziri hao pamoja na manaibu wao ambao
wapo 12 wanawakilisha nchi sita zilizopo ndani ya Jumuiya ya Afrika
madhariki ambazo ni Tanzania ,Kenya,Uganda ,Burundi,Rwanda na Sudan
kusini.
Wakiongea na
waandishi wa habari kwa nyakati tofauti walisema kuwa hawawezi kuendelea
kujadili bajeti wakati mawaziri hao hawapo kwani haita kuwa na maana
sababu mawaziri hao walitakiwa kuwepo na kusikiliza shida za wananchi wa
Afrika mashariki zinazotolewa na wawakilishi wao ili waweze kutoa
ufafanuzi na ikishindikana wakazishughulikie baada ya bunge kumalizika
"tumeamua
kwa umoja kugoma na kusema atutaingia bungeni kuendelea kujadili bajeti
hii wakati mawaziri ambao tulitaraji kuwauliza baadhi ya maswali
ambayo yanahusu bajeti hii ya mwaka 2019/2020 ,sasa tumeamua
kutoendelea hadi pale mawaziri wote watakapo fika"alisema Adamu
Kimbisa
Alisema kuwa
taratibu za mabunge yote duniani zinajulikana na zinasema linapo
jadiliwa bunge la bajeti katika mabunge lolote waziri husika alie
wakilisha bajeti awepo .
"inashangaza
tu kuona naibu waziri mmoja tu tena kutoka nchini Burundi ndio yupo
wengine wote hawapo na walitakiwa wawepo iliwaweze kusikia bunge hili
kwani ni muhimu sana maana linaongelea mapato na matumizi katika mwaka
wa fedha 2019/2020 "alisema Kimbisa
Kwa
upande wake mwenyekiti wawabunge wa Tanzania bunge la jumuiya ya Afrika
mashariki (EALA) Dkt. Abdallah Makame alisema kuwa jumuiya hii iliunda
kwa lengo la ushirikiano na kuwaleta pamoja lakini mawaziri hawa
wanavyokuwa hawaoni kani inavunja moyo wa kuwa na ushirikiano na sisi
kama wabunge tunataka ushirikiano ,ushirikiano wa maneno ,ushirikiano
wa vitendo pamoja na ushirikiano katika hali na mali.
"napenda kusema atutaendelea na kikao chochote cha kujadili bajeti hii mpaka pale mawaziri hawa watakapo kuwepo"alisema Makame
Bunge
hilo linaloendelea ndani ya makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki
yaliopo jiji Arusha limeairishwa kwa siku mbili na linatarajiwa
kuendelea apo kesho iwapo mawaziri wote watakuwepo.
940Picha mbunge wa Tanzania bunge la jumuiya ya Afrika mashariki (EALA)Adamu Kimbisa akiongea na waandishi wa habari mara baada ya bunge hilo kuairishwa.
Wabunge
wa jumuiya ya Afrika mashariki wakijadiliana nje ya jengo la ukumbi wa
bunge la Jumuiya ya Afrika mashariki mara baada ya kutoka katika kikao
cha kujadili bajeti ya mwaka 2019/2020 inayoendelea kujadiliwa katika
bunge hilo picha wa kwanza kulia ni mbunge wa bunge la Afrika mashariki
(EALA)kutoka Tanzania Mariam Ussu pamoja na Pamela Masai
Post A Comment: