Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa akihimiza uwajibikaji kwa watendaji wa Watumishi Housing Company (hawapo pichani) kabla ya kutembelea miradi ya ujenzi wa nyumba za makazi  ya Watumishi wa Umma  zilizopo Gezaulole Kigamboni na Bunju B mkoani Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Company, Dkt. Fred Msemwa akiwasilisha kwa Dkt. Mary Mwanjelwa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa nyumba za makazi  ya Watumishi wa Umma  zilizopo Gezaulole Kigamboni.

Mwonekano wa baadhi ya majengo ambayo ni nyumba zilizojengwa  na Watumishi Housing Company kwa ajili ya makazi kwa Watumishi wa Umma na Wanachama wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii kwa lengo la kuwauzia na kupangisha.

Dkt. Mary Mwanjelwa  akikagua baadhi ya nyumba  za makazi  zilizojengwa  Bunju B mkoani Dar es Salaam kwa ajili ya kuuza na kuwapangisha Watumishi wa Umma na Wanachama wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii.

Dkt. Mary Mwanjelwa akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Company, Dkt. Fred Msemwa mara baada ya kutembelea miradi ya ujenzi wa nyumba za makazi  ya Watumishi wa Umma  na Wanachama wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii zilizopo Gezaulole Kigamboni na Bunju B mkoani Dar es Salaam.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: