Katibu Mkuu Wizara ya
Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Zainab Chaula
akizungumza wakati akifunga Mkutano wa Wakuu wa Vyuo vya Afya vya Serikali uliofanyika
Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya
Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Zainab Chaula
amefungua Mkutano wa Wakuu wa Vyuo vya Afya vya Serikali uliofanyika
Jijini Dodoma.
Katika Mkutano huo Dkt. Zainab Chaula amewataka Wakuu wa
vyuo kuongeza ubunifu katika utoaji huduma kwenye taasisi zao na
kuboresha miundombinu jambo litakalosaidia kuinua kiwango cha elimu
katika maeneo yao.
Kwa upande mwingine, Dkt. Chaula amewataka Wakuu hao wa
vyuo vya Afya kuondoa dhana ya kuitegemea Serikali katika kila jambo ili
kuwaletea Maendeleo, huku akisisitiza uanzishwaji wa vitega uchumi
katika vyuo hivo jambo litalosaidia kupambana dhidi ya ukata wa fedha.
Aidha, Dkt Zainab Chaula amekemea vitendo vya uvunjaji wa
maadili vinavyofanywa na baadhi ya Wakuu wa vyuo ikiwemo suala ya
Rushwa, kufelisha wanafunzi, mambo yanayopelekea kutia doa Maendeleo ya
taasisi hizo.
"Mkuu wa Chuo ni kama mzazi, kuna baadhi ya maeneo unakuta
Mkuu wa chuo anatongoza wanafunzi, wengine wanafukuzisha wanafunzi,
mnaharibu Watoto wa wenzenu, kwa hali hii tutazipata wapi baraka za
Mwenyezi Mungu " alisema Dkt Chaula.
Mbali na hayo, Dkt Zainab amewapongeza Wakuu hao wa Vyuo
kwa Juhudi wanazoendelea kuchukua katika kuboresha vyuo hivo licha ya
changamoto lukuki wanazoendelea kukumbana nazo.
Dkt. Chaula aliendelea kusema kuwa, Serikali inatambua
Juhudi kubwa zinazofanywa na Wakuu wa vyuo vya Afya nchini na kuahidi
kupokea changamoto zote na kuendelea kutafutia ufumbuzi kadiri
inavyowezekana.
Post A Comment: