Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza
wakati alipofungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB kwenye Kituo cha
Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Mei 17, 2019. (Picha na
Ofisi ya Waziri Mkuu)
Mheshimiwa
Majaliwa akiongozwa na baadhi ya viongozi walioshiriki katika Semina
hiyo kuingia kwenye kukumbi wa Simba ili kufungua Semina hiyo. Kutoka
kulia ni Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles
Kicheere, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, Mwenyekiti wa Bodi ya
Benki ya CRDB, Ally Hussein Laay na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Benki ya CRDB, Abdulmajid Musa Nsekela. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Mheshimiwa Majaliwa akiongozwa na baadhi ya viongozi walioshiriki katika Semina hiyo kuingia kwenye kukumbi wa Simba ili kufungua Semina hiyo. Kutoka kulia ni Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Kicheere, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Hussein Laay na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Musa Nsekela. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Musa Nsekela wakati aliopowasili kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) kufungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB, Machi 17, 2019. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Ally Hussein Laay, wa tatu kushoto ni Balozi wa Denmark nchini, Einar Hebogard Jensen na wapili kulia ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Arusha, Rota Sanare. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na viongozi baada ya kufungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB iliyofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Mei 17, 2019. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Ally Hussein Laay, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Musa Nsekela na wa tatu kushoto ni Balozi wa Denmark chini, Einar Hebogard Jensen.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Na Yusuph Mussa, Arusha
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Mei 17, 2019
amefungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Kituo cha
Mikutano cha
Pichani, Mheshimiwa Majaliwa
akiongozana na baadhi ya viongozi walioshiriki katika Mkutano huo,
kuingia kwenye ukumbi wa Simba kufungua Semina hiyo. Kutoka kulia ni
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Kicheere,
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi
ya Benki ya CRDB, Ally Hussein Laay na wa pili kushoto ni Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Musa Nsekela. (Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)Mheshimiwa Majaliwa akiongozwa na baadhi ya viongozi walioshiriki katika Semina hiyo kuingia kwenye kukumbi wa Simba ili kufungua Semina hiyo. Kutoka kulia ni Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Kicheere, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Hussein Laay na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Musa Nsekela. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Musa Nsekela wakati aliopowasili kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) kufungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB, Machi 17, 2019. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Ally Hussein Laay, wa tatu kushoto ni Balozi wa Denmark nchini, Einar Hebogard Jensen na wapili kulia ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Arusha, Rota Sanare. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na viongozi baada ya kufungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB iliyofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Mei 17, 2019. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Ally Hussein Laay, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Musa Nsekela na wa tatu kushoto ni Balozi wa Denmark chini, Einar Hebogard Jensen.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Na Yusuph Mussa, Arusha
WAZIRI
Mkuu Kassim Majaliwa ameitaka Benki ya CRDB kutoa elimu kwa wananchi
kabla ya kutoa mikopo, kwani baadhi ya waliopata mikopo kutoka kwenye
taasisi za fedha wamejikuta wakishindwa kuendesha biashara zao ili
kurejesha mkopo huo, na matokeo yake wananyang'anywa mali zao.
Aliyasema
hayo leo Machi 17, 2019 wakati anafungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya
CRDB iliyofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano jijini Arusha
(AICC), Ukumbi wa Simba.
"CRDB
mnatakiwa kutoa mikopo huku mkieleza matumizi bora ya fedha hizo za
mkopo. Wananchi wengi wanaochukua mkopo huo, hawana elimu ya jinsi ya
kutumia fedha hizo waweze kupata tija kwenye biashara au shughuli zao.
Matokeo yake wanalia kwa kuchukuliwa nyumba zao, mashamba yao, magari
yao, ng'ombe zao na mbuzi zao. Hivyo ni matumaini ya Serikali, mtaanza
kutoa elimu kabla ya kutoa mikopo" alisema Majaliwa.
Majaliwa
alisema moja ya mambo yanafanya taasisi za fedha zinakufa, ni kukosa
usimamizi mzuri kutoka kwa menejimenti na Bodi ya Wakurugenzi. Hivyo
ameitaka Benki ya CRDB kuhakikisha inaboresha utendaji na uwajibikaji.
"Baadhi
ya mashirika yamefilisika kutokana na kukosa utendaji na uwajibikaji.
Na mwaka jana tumefunga benki tano kutokana na kukosa uwajibikaji,
utendaji na Utawala Bora. Mtu yupo pale anataka kuchomoa fedha. Na hiyo
ni kutokana na shughuli zetu kutoratibiwa vizuri. Hatutarajii hilo
kutokea kwenye benki hii" alisema Majaliwa.
Mkuu
wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo alisema kutokana na Jiji la Arusha kuwa
la kitalii, Benki ya CRDB iangalie uwezekano wa kuongeza muda wa
kufanyakazi, ikibidi hata saa nne usiku angalau hata kwa tawi moja.
"Pia
nashauri, kwa vile sasa hivi wajasiriamali wapo wengi, basi CRDB
iangalie namna ya kuwainua wafanyabiashara hawa wadogo kwa kuwawezesha
mikopo, ili watoke hapo kwenye umachinga na kuwa wafanyabiashara wakubwa
kama Dkt. Reginald Mengi" alisema Gambo.
Gambo
alisema utalii wa ndani bado muamko wake ni mdogo, hivyo Benki ya CRDB
iangalie uwezekano wa kutangaza utalii wa nchi yetu kwa kuwapeleka
wanahisa kwenye Hifadhi ya Ngorongoro kila baada ama kabla ya kufanya
Mkutano Mkuu wa mwaka.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Benki ya CRDB Ali Laay alisema huu ni wakati wa wananchi
kuchukua hisa, kwani baadhi ya watu wamewekeza kununua, nyumba, magari,
mbuzi na ng'ombe, lakini uwekezaji mkubwa na endelevu ni wa kununua
hisa, kwani hivyo vingine unaweza kufilisika, lakini wa kununua hisa
kila siku utajiweza kimaisha.
Mkurugenzi
Mtendaji mpya wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela alisema wamejipanga
kuweza kuendesha benki hiyo kwa weledi ili wanahisa waweze kupata faida
na kuona umuhimu wa wao kuwa sehemu ya benki hiyo. Pia kujenga uchumi wa
nchi, uboreshaji huduma kwa wateja, kuongeza matumizi ya kifedha, huku
wakiwa na matawi 263 nchi nzima.
"Lakini
pia tunataka kuongeza ufanisi wa kibiashara, kuboresha mahusiano na
Serikali na wadau wengine. Nia ikiwa kujenga uchumi wa nchi na
uboreshaji huduma kwa wateja. Nia ni kuifanya benki ya kimkakati"
alisema Nsekela.
Akichangia
baadhi ya mada zilizotolewa kwenye semina hiyo, mmoja wa wanahisa
Kapteni Mstaafu Noel Nkoswe kutoka Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa,
alisema kwa sasa hali ya uchumi kwa wananchi mmoja mmoja imeshuka, kwani
wao kama wakulima wa mahindi wameshindwa kupata soko, na sasa
wamehamia kulima alizeti, lakini bado changamoto za kuuza zipo pale
pale.
"Lazima
tuzungumzie kushuka kwa uchumi kwa wananchi wetu, na hata kama Waziri
Mkuu angekuwa bado yupo ukumbini ningemueleza. Hali ni mbaya kwa
wananchi. Wanalima mahindi, lakini bei ni ndogo. Biadhara za wananchi
zinakufa, sio kwa sisi tuliopo vijijini tu, bali hata jijini Dar es
Salaam maduka yamefungwa, kwani tunaona kwenye vyombo vya habari.
"Nawaomba
wenzangu tuache kusifia kila kitu, ni lazima tukae na kujadili uchumi
wa nchi yetu kuona ni namna gani tutajikwamua kutoka hapa tulipo.
Mnanishawishi ninunue trekta la sh. milioni 68 kwa mkopo, lakini
sitaweza kurudisha fedha hizo za mkopo, bali itabidi nikulipe mahindi
ama alizeti, lakini sio fedha, maana sitapata fedha hizo" alisema
Nkoswe.
MWISHO.
Post A Comment: