Baadhi ya washiriki kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo wanawake na vijana wenye nia ya kutaka kugombea nafasi mbalimbali kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa wilaya za Korogwe, Muheza, Handeni na Lushoto, ambapo mafunzo hayo yaliyofanyika Mei 14 na 15, 2019, yameratibiwa na Taasisi ya Tanzania Youth Coalition (TYC) kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU), na kufanyika mjini Korogwe.


Baadhi ya washiriki kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo wanawake na vijana wenye nia ya kutaka kugombea nafasi mbalimbali kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa wilaya za Korogwe, Muheza, Handeni na Lushoto, ambapo mafunzo hayo yaliyofanyika Mei 14 na 15, 2019, yameratibiwa na Taasisi ya Tanzania Youth Coalition (TYC) kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU), na kufanyika mjini Korogwe. Kulia ni mkufunzi Dkt. Ali Fungo.
 Baadhi ya washiriki kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo wanawake na vijana wenye nia ya kutaka kugombea nafasi mbalimbali kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa wilaya za Korogwe, Muheza, Handeni na Lushoto, ambapo mafunzo hayo yaliyofanyika Mei 14 na 15, 2019, yameratibiwa na Taasisi ya Tanzania Youth Coalition (TYC) kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU), na kufanyika mjini Korogwe.

Na Yusuph Mussa, Korogwe


BAADHI ya viongozi wa vyama vya siasa wanadaiwa kuchangia kukosekana kwa wagombea wanaokubalika kwa wananchi, kwani kutokana na sheria kuwa huwezi kugombea bila kupitia kwenye chama, kiongozi wa chama anatumia mbinu kuhakikisha hupati nafasi hata kama umeshinda kura za maoni.


Hayo yamesemwa  (Mei 14) kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo wanawake na vijana wenye nia ya kutaka kugombea nafasi mbalimbali kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa wilaya za Korogwe, Muheza, Handeni na Lushoto, ambapo mafunzo hayo yameratibiwa na Taasisi ya Tanzania Youth Coalition (TYC) kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU), na kufanyika mjini Korogwe.


"Baadhi ya viongozi wa kisiasa kwenye ngazi ya vijiji, kata na wilaya, wanachagua wagombea kwa maslahi yao. Kiongozi anakufuata na kukuuliza vipi upo tayari nikusaidie kupita? unaposhindwa kutimiza matakwa yake, anakuwekea alama za chini wakati wa majina yenu kwenda kuchujwa ngazi za juu, matokeo yake jina lako linakatwa, hata kama wananchi wanakupenda" alisema Majuto Mafiga kutoka kata ya Segera wilayani Handeni.


Naye Upendo Kiangi kutoka Kata ya Mazinde wilayani Korogwe alisema baadhi ya wagombea wa nafasi mbalimbali wanatumia nafasi ya ukoo mkubwa ama uzawa, hivyo ukiwa mgeni, yaani kutoka mkoa mwingine huwezi kupata uongozi.


"Mimi nataka kugombea uongozi kwenye kijiji ama kata yangu ya Mazinde, lakini nashindwa kupata kwa vile kuna mgombea ukoo wake ni mkubwa. Yaani ukoo wake peke yake unatosha kumchagua kuwa kiongozi. Sasa hiyo inakosesha nafasi kwa wengine, hasa ukiwa wa kuja (kutoka mkoa mwingine)" alisema Kiangi.


Twalib Shafii kutoka Kata ya Masuguru, Wilaya ya Muheza alisema angalau wana imani na utawala wa Awamu ya Tano, vitendo vya rushwa vitapungua sana, kwani kwenye chaguzi zilizopita, baadhi ya wagombea wa nafasi mbalimbali walipita kwa rushwa, hivyo anaamini vyombo vya dola vitakuwa makini kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu mwakani.


Mkufunzi Dkt. Ali Fungo alisema wakati wa uchaguzi ni lazima mgombea aheshimu maadili ya chama chake. Pia anatakiwa kutoa ahadi zenye uhalisia na mahitaji ya wenyeji wa eneo husika.


"Huwezi kufanya kampeni kata ya Mashewa (Korogwe) halafu ukaahidi kuwajengea kiwanda, wakati wao ni wakulima, na wanahitaji zana za kilimo ili kufikia mahitaji yao" alisema Dkt. Fungo.


Mratibu wa Mradi wa Kuwawezesha Wanawake na Vijana (WYPRE) katika Mkoa wa Tanga, ambao upo chini ya TYC Yahaya Kitogo alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwaandaa wanawake na vijana kugombea nafasi mbalimbali kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.


MWISHO.
Share To:

Post A Comment: