MKUU wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro akizungumza wakati wa wiki ya mlipa kodi kwenye soko la Tangeru Mkoani Arusha

Kaimu Meneja wa TRA  Irene Donald akizungumza

 Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Mamlaka ya  mapato TRA mkoani Arusha imetoa onyo kwa baadhi ya vishoka wanaowatapeli wafanyabiashara kupitia mgongo wa TRA waache kufanya hivyo mara moja kwani watachukulia hatua kali za kisheria kwani wanakwamisha ulipaji kodi kwa hiari.
Kaimu Meneja wa TRA Irene Donald amesema hayo jana katika soko la Tengeru ambapo alizungumza na walipa kodi katika wiki ya mlipa kodi ,ambapo amesema kuwa kuna baadhi ya watu wanaofahamika kama vishoka ambao hufika TRA na kufanya udanganyifu kwa wafanyabiashara kwa lengo la kujipatia faida huku wakiwaumiza wafanyabiashara.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru  Jerry Muro amesema kuwa wafanyabiashara wanapaswa kulipa kodi kwa hiari ili kuchangaia maendeleo ya nchi na kuiwezesha serikali kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi wake.
Kwa upande wao wafanyabiashara waliofika  kupata elimu ya mlipa kodi Magreth Pallangyo amelalamikia uchafu wa soko la tengeru licha ya kulipa ushuru kwa Halmashauri hiyo hivyo wameiomba serikali itatue changamoto hiyo ili waweze kulipa kodi stahiki.
Share To:

Post A Comment: