Mpenzi wa msanii Diamond Platnumz, Tanasha amesema kuwa si rahisi kwa yeye kubadilisha dini kisa mahusiano  ila mapenzi yake na muimbaji huyo  yako pale pale.

Tanasha amefunguka hayo alipokuwa akihojiwa na Block 89 ya Wasafi FM kwa kueleza kuwa kila mmoja anaheshimu dini ya pande zote mbili.

"Mara ya kwanza nilikuwa na wasiwasi wakati tunaanza uhusiano, Diamond Platnumz ni star na nini. Naheshimu dini yake na yangu pia, sitabadilisha dini lakini mapenzi yatabaki" amesema Tanasha. 
Share To:

msumbanews

Post A Comment: