Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbas amesema hakuna agizo la Serikali linalolazimisha mfanyakazi wa Serikali kuwa na laini ya TTCL isipokuwa viongozi wanaowekewa vocha za Serikali kwamba ni muhimu kuwa na laini hizo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo amesema taarifa inayosambaa kwenye mitandao kuhusu hilo ni ya upotoshaji na kuwataka wananchi kuipuuza.

"Hakuna agizo la serikali linalolazimisha mfanyakazi wa serikali kuwa na laini ya TTCL, isipokuwa viongozi wanaowekewa vocha za serikali ni muhimu kuwa na laini hizo." amesema.

 Chini taarifa hiyo iliyokanushwa.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: