NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) kushoto akipata futari na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly katikati wakati futari iliyoandaliwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) kwa ajili ya wafanyakazi na majirani zao kwa ajili ya kujenga mshikamano na umoja miongoni mwao.
 NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) kushoto akipata futari na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly katikati wakati futari iliyoandaliwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) kwa ajili ya wafanyakazi na majirani zao kwa ajili ya kujenga mshikamano na umoja miongoni mwao.
 NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) kushoto akipata futari na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly katikati wakati futari iliyoandaliwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) kwa ajili ya wafanyakazi na majirani zao kwa ajili ya kujenga mshikamano na umoja miongoni mwao.

 NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) kushoto akipata futari na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly katikati wakati futari iliyoandaliwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) kwa ajili ya wafanyakazi na majirani zao kwa ajili ya kujenga mshikamano na umoja miongoni mwao.
 Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gispson George kushoto akiwa na Katibu wa Naibu Waziri wa Maji Lichela katikati na Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Hassani Nyange wakipata futari hiyo
 PRO wa Tanga Uwasa Dorrah Killo akishiriki kugawa futari
 Sehemu ya wafanyakazi na majirani wakipata futari hiyo


NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema wizara hiyo inatarajiwa kupeleka miradi zaidi ya mitatu mikubwa mkoani Tanga kwa maana ya ile ya miji 28 Tanzania Bara na mmoja wa Visiwani.

Aweso aliyasema hayo leo wakati halfa ya futari iliyoandaliwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) kwa ajili ya wafanyakazi na majirani zao kwa ajili ya kujenga mshikamano na umoja miongoni mwao.

Alisema kwamba miradi hiyo itakwenda kwenye wilaya za Handeni, Muheza na Pangani ambazo zitanufaika nao ili kuweza kuondosha changamoto za huduma hiyo zilizopo kwenye maeneo yao .

“Sisi kama Wizara tumeona kazi nzuri inayofanywa na Tanga Uwasa kwani hivi sasa wanatoka Tanga Jiji wanaenda maeneo mengine ikiwemo Lushoto wanasimamia miradi, Muheza na Handeni hivyo sisi tutaongeza nguvu”Alisema Naibu Waziri huyo

Aidha alisema watahakikisha wanawezeshwa kuhakikisha miradi hiyo inakamilika ikiwemo kuwasimamia wakandarasi wanayoitekeleza ili miradi hiyo iweze kutekeleza kwa waledi mkubwa na hatimaye kuweza kuondosha changamoto zilizopo kwenye maeneo husika.

Awali akizungumza katika futari hiyo Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly alisema hafla hiyo ilikuwa ni kuwafuturisha wafanyakazi wao waislamu na majirani kwa ajili ya kujenga umoja miongoni mwao.

Alisema kwa sababu wamekuwa wakikaa pamoja kwa umoja lengo kuwakumbuka waislamu waliofunga kwenye kipindi hiki cha mfungo mtukufu wa ramadhani kwani suala la kufunga ni muhimu sana kwa ajili ya kufanya ibada.

Hata hivyo aliwatakia kilala heri waislamu katika mfungo kwa sababu unawapa nguvu zaidi ya kuishi maisha mema zaidi na kuweza kushindana na vishawishi.

Mwisho.
Share To:

Post A Comment: