Kaimu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto(Katikati) akiangalia
bidhaa za Wajasiriamali wa Wilaya ya Ilala katika uzinduzi wa Jukwaa
la Wanawake wa Kata ya Segerea (Picha na Heri Shaaban)
Kaimu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbila moto akikata utepe
kuashiria uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Segerea Dar es salaam
leo(kushoto)Ofisa maendeleo Manispaa ya Ilala Fransica Makoye(kushoto)
Mwenyekiti wa Jukwaa wa kata ya segerea Julieth Banigwa(Picha na Heri
Shaaban)Katibu wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Mkoa Dar es Salaam Husna Shechonge akiongea katika uzinduzi wa Jukwaa segerea (NA.HERI SHAABAN)
Mratibu wa Dawati la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Wilaya ya Ilala
Georgis ASENGA akizungunza na katika uzinduzi wa Jukwaa kata ya Segerea
(Picha na Heri Shaaban)
NA HERI SHABAN
MANISPAA ya Ilala imesema inatarajia kutenga eneo la Mnazi Mmoja kwa ajili ya Biashara za Wajasiriamali.
MANISPAA ya Ilala imesema inatarajia kutenga eneo la Mnazi Mmoja kwa ajili ya Biashara za Wajasiriamali.
Hayo yalisemwa na Kaimu Meya wa Manispaaa ya Ilala Omary
Kumbilamoto wakati wa kuzindua Jukwaa la Wanawake la Uwezeshaji Wanawake
Kiuchumi Kata ya Segerea Wilayani Ilala Dar es salaam .
"Manispaa yangu ya Ilala imetenga eneo la uwanja mdogo
Mnazi Mmoja litatumika kwa ajili ya bidhaa mbalimbali za Wanawake pamoja
na eneo la Ocen road Wajasiriamali wa Wilaya ya Ilala watakuwa wanauza
biashara zao" alisema Kumbilamoto.
Aidha alisema Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala kwa
Kushirikiana na Mkurugenzi wa halmashauri wanaweka utaratibu mzuri
kuboresha eneo hilo ili liwe sehemu ya kutuo cha biashara kwa wilaya ya
Ilala.
Kumbilamoto aliwataka Wanawake kuchangamkia fursa kujikwamua kiuchumi kila mtu ajishughulishe
.
Alisema Manispaa ya Ilala inatarajia kutoa mikopo awamu ya
tatu Mei 30 mwaka huu dhumuni kila mtu aweze kupata mikopo hiyo akuna
riba wala kizuiz.
"Halmashauri yetu imejipanga vizuri inatarajia kutoa mikopo
shilingi bilioni 2 wananchi wa Manispaa ya Ilala wacha kusikiliza radio
mbao fedha zipo bila riba "alisema.
Kwa upande wake Katibu wa Jukwaa Mkoa Dar es Salaam Husna
Shechonge alisema Majukwaa ya Wanawake hayana fedha dhumuni lake
kutambua nafasi zetu tulizonazo .
Husna alisema majukwaa ya wanawake yote ameadhishwa sio kwa ajili ya dhumuni la mikopo majukwaa ya uwezeshaji Wanawake Kiuchumi hayana mikopo.
Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi
kata ya Segerea Julieth Banigwa alisema jukwaa la Segerea lina vikundi
17 vya Wajasiriamali vilivyosajiliwa na vingine vipo katika hatua za
usajili .
Banigwa alisema jukwaa hilo limewawezesha kutengeneza
mtandao wa biashara ambapo imewasaidia kupanua wigo wa masoko na bidhaa
zinazozalishwa katika vikundi.
Akielezea changamoto alisema wana vikundi kutokuwa na elimu ya ufungashaji na udhibiti wa ubora .
Pia ukosefu wa masoko ya uhakika ya bidhaa zinazozalishwa na wana Jukwaa katika vikundi.
Mwisho
Post A Comment: