Kamishna Mkuu wa TRA, Charles Kichere akizungumza
Na  Ferdinand Shayo,Arusha.
Kamishna Mkuu wa Tra, Charles Kichere  amefanya ziara ya kutembelea maduka jijini Arusha  na kutoa elimu kwa wafanyabiashara ikiwemo kukagua mashine za kielektroiniki pamoja na kusikiliza changamoto za wafanyabiashara hao na kuzipatia ufumbuzi.
Kichere amefika katika maduka mbalimbali yaliyopo jijini Arusha na kuzungumza na wafanyabiashara hao ana kwa ana ikiwa ni mpango wa kuwafikia wafanyabiashara na kuwasikiliza katika wiki ya elimu kwa mlipa kodi innayoendelea mkoani Arusha.
Aidha amewataka wafanyabiashara hao kushirikiana bega kwa began a mamlaka hiyo na kulipa kodi kwa hiyari ili kuchangia maendeo ya taifa .
Kamishna huyo ametembelea soko la Ngaramtoni na kuzungumza na Wafanyabiashara ambao walitoa kero zao na kuzitolea majibu ikiwa ni utekelezaji wa dhana ya kutoa elimu kwa walipa kodi.
Kwa Upande wake Mfanyabiashara Swalehe Mkwizu ametoa mapendekezo yake ya kuitaka Tra iongeze wigo wa kukusanya kodi katika vyanzo vipya ili kuongeza mapato badala ya kutegemea vyanzo vilivyopo
Salehe amesema kuwa kwa sasa TRA inafanya kazi nzuri ya kuhakikisha kuwa inawahudumia vyema wafanyabiashara kwa haraka na kwa ufanisi mkubwa hivyo kupunguza msongamano  wa watu katika ofisi zao.
Mfanyabiashara wa Duka la Pembejeo Godlisten Jackson ameiomba TRA uwapunguzie kodi kutokana na mlolongo wa kodi walizonazo kutoka katika mamalaka nyingine ili waweze kufanya biashara hiyo na kuleta tija.
Share To:

Post A Comment: