Balozi
wa Kenya Nchini Tanzania Dan Kazungu akitoa ushauri kwa Wakala wa
Misitu Tanzania (TFS) wilaya ya Kalambo juu ya kuboresha eneo hilo la
Maporomoko.
Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Dan Kazungu (kushoto) akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (kulia) wakati walipofika kwenye sehemu ya kwanza ambapo maporomoko hayo hayaonekani kwa ufasaha (nyuma yao).
Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Dan Kazungu (kulia) akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (kushoto) wakati wakiteremka ngazi za kuelekea kwenye kina cha maporomoko ya Kalambo. (Kalambo Falls)
Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Dan Kazungu (kushoto) akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (kulia) wakati walipofika kwenye sehemu ya kwanza ambapo maporomoko hayo hayaonekani kwa ufasaha (nyuma yao).
Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Dan Kazungu baaada ya kufika eneo ambalo unaweza kuyaona maporomoko hayo vizuri.
Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Dan Kazungu (kushoto) akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (kulia) wakati walipofika kwenye sehemu ya kwanza ambapo maporomoko hayo hayaonekani kwa ufasaha (nyuma yao).
Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Dan Kazungu (kulia) akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (kushoto) wakati wakiteremka ngazi za kuelekea kwenye kina cha maporomoko ya Kalambo. (Kalambo Falls)
Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Dan Kazungu (kushoto) akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (kulia) wakati walipofika kwenye sehemu ya kwanza ambapo maporomoko hayo hayaonekani kwa ufasaha (nyuma yao).
Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Dan Kazungu baaada ya kufika eneo ambalo unaweza kuyaona maporomoko hayo vizuri.
Sehemu ya Maporomoko ya Kalambo (Kalambo Falls)
Balozi wa
Kenya nchini Tanzania Dan Kazungu amewaomba wawekezaji kutoka kila pande ya
dunia kujitokeza kwa wingi kuwekeza kwa kujenga hoteli na nyumba za kupumzikia
wageni katika eneo linalozunguka maporomoko ya Kalambo (Kalambo Falls) yaliyopo
katika Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa.
Amesema kuwa
eneo hilo ni zuri kwa wanafamilia kulitumia katika siku za mapumziko, siku za sikukuu
na pia kujitokeza ili kuyaona maajabu hayo ambayo yametambuliwa na Shirika la
umoja wa mataifa la Elimu, Sayansi, na Utamaduni (UNESCO) kuwa ni urithi wa
dunia.
“Tunaomba
wawekezaji waje hapa kwa wingi, hapa kuna kivutio ambacho kimejulikana na umoja
wa mataifa UNESCO kama hifadhi ya urithi wa dunia, mje wawekezaji hapa, pahali
ambapo siku za mwisho wa wiki watu wanaweza kuja kujipumzisha ama siku za sikukuu
kuja na familia yao kwaajili ya “picnic”, wanajenga “lodges” lakini tunaomba “lodges”
zijengwe nyingi zaidi za hadhi ya ubora wa juu zaidi ili tufurahie na familia
zetu,” Alisema.
Balozi Kazungu
ameyasema hayo alipotembelea maporomoko ya kalambo katika ziara yake ya siku
moja Mkoani Rukwa iliyolenga kutafuta fursa za uwekezaji katika maeneo mbalimbali
ya Mkoa huku akitembelea kiwanda cha Nyama cha SAAFI pamoja na ujenzi wa upanuzi
wa uwanja wa ndege wa Sumbawanga.
Aidha, Balozi
Kazungu alitoa ushauri kwa wakala wa misitu Tanzania wanaoshughulika na
uhifadhi wa msitu wa Kalambo pamoja na kuimarisha miundombinu ya maporomopko
hayo kuona uwezekazo wa kuweka nyaya pamoja na vigari vitakavyopita kwenye
nyaya hizo ili watalii waweze kuyaona maporomoko hayo vizuri zaidi pamoja na
msitu huo.
Wakati
akisoma taarifa ya maporomoko hayo ya Kalambo, Kaimu Meneja wa Wakala wa Misitu
Wilaya ya Kalambo Helman Ndanzi amesema kuwa pindi ujenzi wa ngazi za
kushukukia kutoka maporomoko yanapoanzia hadi kufikia sehemu maji yanapodondokea
utakapokamilika, ngazi hizo zitakuwa na urefu wa mita 1277 na kugharimu
shilingi 852,789,066.70.
“Changamoto
zilizopo ni kutotangazwa vya kutosha maporomoko hayo hali inayopelekea
kutojitokeza kwa wawekezaji katika eneo hilo ambalo mawasiliano ya simu pia
bado ni tatizo na hivyo tunaiomba mitandano mbalimbali ya simu kujitokeza
kuweka minara katika maeneo haya ili mawasiliano yawe rahisi,” Alisema.
Wakati huo
huo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alimhakikishia Balozi huyo kuwa
mkoa umejipanga kuhakikisha unakamilisha miundombinu inayohitajika ili
kuwarahisishia wawekezaji kutekeleza shughuli zao kwa urahisi na hatimae kuinua
uchumi wa wananchi katika mkoa lakini pia uchumi Tanzania kwa ujumla.
“Sisi tupo
kwenye mpango ule wa viwanja vya ndege vile vinne, kuna kiwanja hiki cha
Sumbawanga, Tabora, Shinyanga pamoja na Kigoma, karibu kila kitu kipo tayari
kimazingira, vitu vyote vinavyotakiwa kufanyika kabla ya kuanza upanuzi wa
uwanja tayari vimekwishafanyika, mhandisi mshauri yupo, mkandarasi yupo,
mikataba tayari, fidia kwa wananchi waliohusika nae neo la upanuzi tayari, kila
kitu kipo tayari, bado serikali haijaruhu lakini bila ya shaka wakati wowote
ruhusa itatoka,” Alisisitiza.
Maporomoko
ya Kalambo ni maporomoko ya pili kwa urefu kutoka maji yanapoanzia kumwagika
hadi yanapodondokea kwa mita 235 na upana wa mita kuanzia 3.6 hadi mita 18
(single drop waterfall) ambapo maporomoko ya kwanza ni ya TUGELA yaliyopo
Afrika ya Kusini yenye urefu wa mita 947.
Post A Comment: