Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro akizungumza na Mganga mkuu wa Halmashauri ya Arusha Dc Dokta Petro Mboya mara baada ya kutoka kuwatembelea majeruhi wa ajali iliyotokea Odonyosambu.
Watanzania wametakiwa kuacha kukurupuka na kuandika vitu ovyo na zinazozua taaruki pindi tatizo linapotokea badala yake wasubiri taarifa kutoka maamlaka husika.
Hayo yamesemwa leo na mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro wakati alipokuwa akiongea na vyombo vya habari mara baada ya kuwatembelea majeruhi wa ajali ya gari iliotokea jana katika eneo la Odonyosambu jijini hapa .
Ambapo mkuu huyo wa wilaya alianza kwa kukanusha taarifa ambazo zinasambaa ovyo mitandaoni na sehemu mbalimbali zinazodai kuwa katika ajali iliotokea jana watu nane wamefadiki duniana watu hao ni wa nchi jirani ya Kenya kitu ambacho sicho cha kweli kwani katika ajali hiyo watu wawili tu ambao majina yao hayajatambulika ndio wamefariki dunia
Aliwataka wananchi waache kusambaza na kuandika taarifa ambazo zinazua taaruki na zinasumbua watu mbalimbali ambao wanataka kujua kitu ambacho kinaendelea
"sisi tumefika tumejirizisha miiili tulioipokea ni miili miwili tu ,na majeruhi ni wanne na baadhi ya ndugu wa majeruhi kutoka nchi jirani wapo hapa wanaangalia ndugu zao na pia hata hawa majuruhi wa hapa nchini pia wapo hapa wanawaangalia najitiada za kunusuru maisha yao zinaendelea na sisi kama serikali tunapambana kuhakikisha kila linalowezekana kuokoa maisha yao "Alisema Muro
Aidha aliwataka wananchi wa Arumeru na mkoa wa Arusha kwa ujumla iwapo watataka kufanya matukio yeyote yale kama kusanyiko lolote linalolenga shughuli za pembezoni ya barabara lazima tukio hilo liripotiwe kwa serikali ili serikali iwaandalie vitu vya usalama na watu waache kufanya vitu kwa mazoea kwani serikali hii haiendeshi kwa mazoea bali kwa kufuata sheria
kwa upande wake mganga mkuu wa hospitali ya halmashauri ya Arusha Petro Mboya akiongea na waandishi wa habari alisema kuwa wamepokea miili miwili ya marehemu ambayo bado majina yao hayajatambulika pamoja na majeruhi wa nne ambao kati yao mmoja yupo katika hali mbaya kwani aliumia zaidi katika maeneo ya kichwa.
"hospitali yetu ya Selian lutheran hospital tumepokea majeruhi wanne ambao wametokea katika ajali iliyotokea oldonyosambu na katika hao wanne wawili wameumia vichwa na wapo chumba maututi mmoja ameumia uti wa mgongo ili huyu mmoa aliyeumia kichwa sana tumempa rufaa ya kwenda kumuona daktari bigwa wa mfumo wa fahamu,pia tulipokea maiti mbili ambazo tumeziifadhi katika vyumba vyetu vya kuhifadhia maiti hapa hapa hospitalini kwetu"alisema Mboya
Post A Comment: