Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Maafa  Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe akifafanua umuhimu wa Kamati za Usimamizi wa Maafa wakati wa Mafunzo ya Usimamizi wa Maafa mjini Musoma, tarehe 18 Aprili, 2019, Mafunzo hayo yaliratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa shughuli za maafa,
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Maafa Mkoani Mara,  wakifuatilia Mafunzo ya Usimamizi wa Maafa mjini Musoma, tarehe 18 Aprili, 2019, Mafunzo hayo yaliratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa shughuli za maafa.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima akifafanua umuhimu wa Kamati za Usimamizi wa Maafa wakati wa Mafunzo ya Usimamizi wa Maafa mjini Musoma, tarehe 18 Aprili, 2019, Mafunzo hayo yaliratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa shughuli za maafa, kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara hiyo, Kanali Jimmy Matamwe.

Baadhi ya wananchi walioalikwa kutoka katika Halmashauri za wilaya mkoani Mara,  wakifuatilia Mafunzo ya Usimamizi wa Maafa mjini Musoma, tarehe 18 Aprili, 2019, Mafunzo hayo yaliratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa shughuli za maafa.
Mratibu wa Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Maafa, Charles Msangi  akifafanua umuhimu wa Kamati za Usimamizi wa Maafa wakati wa Mafunzo ya Usimamizi wa Maafa mjini Musoma, tarehe 18 Aprili, 2019, Mafunzo hayo yaliratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa shughuli za maafa.
Mkuu wa Wilaya ya Butiama ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya Mkoa wa Mara, Bi. Annarose Nyamubi, akieleza umuhimu wa Kamati za Usimamizi wa Maafa wakati wa Mafunzo ya Usimamizi wa Maafa mjini Musoma, tarehe 18 Aprili, 2019, Mafunzo hayo yaliratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa shughuli za maafa.
Na. OWM, MUSOMA.
Wajumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Maafa Mkoani Mara wameiomba ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa maafa kuwajengea uwezo wa  kuunda kamati za Usimamizi wa Maafa mkoani humo. Wajumbe hao wamebainisha kuwa wanataka kamati hizo ziundwe kuanzia ngazi ya kijiji hadi ngazi ya mkoa ili mkoa huo uwe na uwezo wa kujiandaa, kuzuia, kukabili na kurejesha hali kama maafa yatatokea.
Kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa maafa Na. 7 ya mwaka 2015, inaainisha  majukumu ya  kamati za usimamizi wa Maafa kuanzia ngazi ya Kijiji hadi mkoa, ambapo kwa mujibu wa sheria hiyo, jukumu la msingi ni kutafuta rasilimali kwa ajili ya usimamizi wa maafa katika ngazi husika, pamoja na  Kuratibu na kusimamia shughuli za usimamizi wa maafa na operesheni za dharura ndani ya Kijiji  wilaya au mkoa. Pia kutoa taarifa za tahadhari ndani ya eneo husika, hivyo kila mkoa hauna budi kuwa na kamati hizi.
Akiongea wakati akifungua mafunzo ya Usimamizi wa Maafa mjini Musoma, tarehe 18 Aprili, 2019, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima, amesema kuwa yeye na wajumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya mkoa wameamua kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Idara ya Uratibu Maafa, ili wawejengee uwezo utakao wawezesha kuanzisha kamati hizo kuanzia ngazi ya Kijiji, ili  Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya mkoa ambayo  ilianzishwa rasmi kisheria kwa ajili ya  kumshauri Mkuu wa mkoa masuala ya Usimamizi wa maafa iweze kumshauri kwa weledi na  kwa wakati. 
“Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu Maafa ikishatujengea uwezo sisi jukumu letu ni moja tu, ni kuhakiksha tunajiimarisha juu ya usimamizi wa maafa kuanzia ngazi ya kijiji ili haya majanga ya Upepo mkali, Ukame, Ajali za vyombo vya usafiri wa majini na nchi kavu, moto, Uharibifu wa mazao unaofanywa na tembo, tuwe na uwezo wa kuyazuia au kupunguza madhara yake  pindi yanapotokea  mkoani hapa na hatutapata vifo, uharibu wa mali na ulemavu wa kudumu kwa wananchi” Amesisitiza Malima.
Naye, Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Maafa  Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe, amefafanua kuwa ili kamati hizo ziwe na ufanisi katika usimamizi wa shughuli za maafa zinapaswa  kuandaa Mkakati wa Kupunguza madhara  ya maafa pamoja na Mpango wa kujiandaa na kukabili maafa.
“Ofisi ya waziri Mkuu tutaendelea kuendesha mafunzo haya  ili kuzijengea uwezo kamati hizi ambazo ni chombo cha kisheria hapa nchini kwa ajili ya kutathimini na kutekeleza masuala ya kitaalam kuhusu usimamizi wa maafa, kuzuia na kupunguza madhara ya majanga ya aina zote katika mkoa lakini mkishapata mafunzo haya hakikisheni mnaweka masuala y amaafakatika mipango yenu ya maendeleo.”
Mafunzo hayo yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa shughuli za maafa, yamehudhuriwa na wajumbe wote wa Kamati ya Usimamizi wa maafa wa mkoa pamoja  kwa kuzingatia Kifungu cha 13 cha sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 7 ya mwaka 2015,  pamoja na baadhi ya wananchi wa kawaida walioalikwa katika kikao  mafunzo hayo. . 
MWISHO.
Share To:

Post A Comment: