Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly akizungumza na watumishi wa mamlaka hiyo mara baada ya kufanikiwa kupata tuzo hiyo kulia ni
 Afisa Rasilimali Watu wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Haika Ndalama akizungumza wakati wa halfa hiyo
Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo Dorrah Killo  akizungumza wakati wa halfa hiyo

  Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly akiwa amebebwa na watumishi wa mamlaka hiyo wakimpongeza baada ya kupata tuzo hiyo
 Watumishi wa mamlaka hiyo wakiwa na tuzo hiyo
  Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly kushoto ambaye amevaa koti akiwa na watumishi wa mamlaka hiyo wakisheherekea ushindi wa tuzo hiyo
 Watumishi wa Mamlaka hiyo wakicheza kwa furaha baada ya kupata tuzo hiyo
 Watumishi wa mamlaka hiyo wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye halfa hiyo
 Watumishi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye halfa hiyo
 Msafara wa magari na pikikpiki ukitokea eneo la Pongwe Jijini Tanga wakielekea Ofisi za Mamlaka ya Maji Jijini Tanga mara baada ya mapokezi ya tuzo hizo



MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) imepata tuzo kwa kuwa mamlaka bora katika utoaji wa huduma za maji safi kwa mamlaka za mikoa 25 Tanzania kwa mwaka 2017/2018.

Tuzo hiyo ilitolewa na Mamlaka ya Udhibiti Nishati na Maji nchini (EWURA) kutokana na utendaji kazi wao na utoaji wa huduma baada ya kufanya tathimini na hivyo kujikuta wakifanikiwa kuigia kwenye nafasi hiyo ya kuny’akua tuzo hiyo.

Akizungumzia namna walivyopokea tuzo hiyo baada ya mapokezi makubwa yaliyoanzia eneo la Pongwe Jijini Tanga Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly alisema wanafurahi kutokea tuzo hiyo kmuwa mamlaka bora katika huduma ya maji safi kati ya mamlaka 25 Tanzania bara ni faraja kubwa sana kwao.

Alisema wameipata tuzo hiyo kwa sababu wamekuwa na nia ya kuipata kutokana na ufanisi mkubwa wa kufanya kazi kwa bidii kwa maarifa huku wakijua vigezo vinavyotakiwa na vigezo kwa ujumla wake ni ubora wa huduma kwa wananchi wanapata maji muda wa kutosha na maji bora.

Alisema pia ni kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama maji kwa kuwafikia watu wengi iwezekanovyo huku wakipunguza upotevu wa maji ambayo vimechangia wao kuonekana mamlaka bora ya kwanza Tanzania bara kutoa huduma ya maji safi 2017/2018,

Mkurugenzi huyo alisema baada ya kupata tuzo hiyo hivi sasa mikakati yao ni kuendelea kujipanga kutambua jinsi vigezo vinafanyiwa kazi ili kupata mamlaka bora kila mwaka kutokana na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

“Tumejipanga na Tutatekeleza yale yanafanyika kwenye vile vigezo tuendelee kubaki kuwa mamlaka bora Tanzania bara na ulimwengu mzima kama ilivyo malengo yetu “Alisema Mkurugenzi huyo.

Awali akizungumza katika halfa hiyo Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo Dorrah Killo alisema baada ya kupata tuzo hiyo wataendelea kupambana kuhakikisha wanaendelea kung’ara katika utoaji wa huduma hapa nchini

“Tukienda mwakani vigezo zinaweza kuwa vikubwa hivyo tutaendelea kujipanga lakini niwaambie kwamba tumewatupa mbali sana wenzetu waliokuwa karibu nasi..hii inatokana na jitihada kubwa za bodi ya wakurugenzi,uongozi na wateja wao”Alisema Afisa Uhusiano huyo.

Alisema suala linguine ni kuwahudumia wateja wao vizuri kwani bila kuwahudumia wateja na kutoa elimu nzuri kwao wasingeweza kufikia hatua hiyo wanashaukru wateja wao na wafanya kazi kwa bidii washirikiana wapendani ili kufikia malengo yao.

Mwisho.

Share To:

Post A Comment: