Mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Wanawake Tanzana Bara maarufu kama Serengeti Lite Women’s Premier League unatarajiwa kuanza kutimua vumbi siku ya Jumamosi, Machi 9 2019.

Mwenyekiti wa Kamati ya Soka la Wanawake, Amina Karuma amesema wanatarajia kuona mzunguko wa pili unakuwa na ushindani kwa timu zote na hatimaye kupata bingwa anayestahili.

Karuma aliipongeza udhamini uliofanywa na Kinywaji cha Serengeti Premium Lite ambao pamoja na mambo mengine umewezesha kuifanya ligi kuwa na ushindani mkubwa na kuleta mvuto wa aina yake.

“Ligi Kuu ya Wanawake ya Serengeti Premier League imeweza kuleta ushindani mkubwa baina ya timu zinazoshiriki na hata ukitazama matokeo unaweza kuona ni jinsi gani ambavyo ligi hii imekuwa na msisimko wa aina yake,” alisema   

Aliongeza kuwa katika kuhakikisha mzunguko wa pili unakuwa bora Zaidi, imefanyika semina ya viongozi wa klabu na Waamuzi Wanawake ili kuwajengea uwezo zaidi.

Kwa upande wake, Ofisa Masoko wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) ambao ni wadhamini wakuu wa Ligi hiyo, George Mango alisema kudhamini ligi hiyo kupitia kinywaji chake cha Serengeti Lite kumelenga kuongeza hamasa na kuleta ushindani wa ligi hiyo ya wanawake.

“Katika mzunguko wa kwanza tumeshuhudia hamasa na ushindani mkubwa miongoni mwa timu zinazoshiriki ligi hii hivyo ni matarajio yetu kwamba mzunguko huu wa pili utakuwa bora zaidi kwa timu zote ili kuongeza zaidi ari ya ushindani,” alisema.

Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) kupitia kinywaji cha Serengeti Lite imeweza kuwekeza jumla ya Sh450 Milioni kama ufadhili wa ligi hiyo ya wanawake nchini kwa kipindi cha miaka mitatu kama sehemu ya kuendeleza michezo hususan mpira wa miguu nchini.

Aidha, SBL imekuwa ikitilia mkazzo uendelezaji wa michezo nchini hasa katika mpira wa miguu ambao mbali na kupendwa na watu wengi umekuwa chachu katika kuinua vipaji mbalimbali nchini.

TIMU ZA LIGI KUU YA WANAWAKE (SWPL) 

1. KIGOMA SISTERZ- KIGOMA 
2. SIMBA QUEENS – DSM
3. ALLIANCE GIRLS –MWANZA
4. BAOBAB QUEENS – DODOMA
5. MLANDIZI QUEENS – PWANI
6. JKT QUEENS – DSM
7. PANAMA – IRINGA 
8. EVERGREEN –DSM
9. MARSH ACADEMY – MWANZA
10. MAPINDUZI QUEENS – NJOMBE 
11. YANGA PRINCESS –DSM
12. TANZANITE – ARUSHA.


Cliford Mario Ndimbo 
Afisa Habari na Mawasiliano,TFF
Machi 8,2019
Share To:

Post A Comment: