1
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mh. Daniel Chongolo mkoani Dar es salaam akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye kituo cha Polisi cha Mbweni baada ya kufanya doria na kukamata magendo ya vitu mbalimbali vilivyokuwa vikivushwa kutoka Zanzibar kuja Tanzania Bara.
Vitu vilivyokamatwa katika doria hiyo ni Sukari ya viwandani mifuko 75, Madumu ya mafuta ya kula 25 na Pikipiki 2, vitu hivyo vimekuwa vikivushwa na Boti na kupokelewa na Ngombe waliopata mafunzo maalum ambao kila mmoja anao uwezo wa kuchukua mifuko 20 ya sukari na madumu kadhaa ya mafuta ya kula kutoka baharini ufukweni mpaka nchi kavu na kupeleka kwenye maghala wanayohifadhia mizigo hiyo moja kwa moja kwa maelekezo wanayopewa na wamiliki wa ng’ombe.
Watu waliokamatwa wakituhumiwa kujihusisha na uvushaji wa magendo hayo ni Ally Haruna Mnyamzwezi mkazi wa Mbweni jijini Dar es salaam , Chauka Jonas Mwendesha Bodaboda mkazi wa Mbweni Jijini Dar es salaam , Hamis Juma Mnyamwezi Mkazi wa Mbweni Jijini Dar es salaam  na mwendesha Bodaboda na Hemedy Ally Mshirazi Kondakta mkazi wa Mbweni jijini Dar es salaam.
Mh. Daniel Chongolo amesema kama mwawakilishi wa Rais na watetezi wa watanzania akishirikiana na jeshi la polisi hawatakubali watu wachache waangamize wananchi kwa kuingiza bidhaa zisizofaa kwa matumizi ya binadamu,  Tutapambana nao kikamilifu na tutahakikisha tunakomesha hii biashara haramu ya bidhaa zisizokuwa na viwango na zisizolipiwa kodi kuingizwa nchini.
Amesema “Tutahakikisha tunavunja hizi bandari bubu zote katika fukwe za bahari ya hindi hasa maeneo ya kuanzia Kawe, Mbweni kwenda  katika mpaka wa Bagaoyo na Dar es salaam ili  kukomesha biashara hii”, Sukari iliyokamatwa ni ile inayotumiaka viwandani ambayo haifai kwa matumizi ya binadamu.
2
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mh. Daniel Chongolo mkoani Dar es salaam akisisitiza jambo wakati akitangaza kukamatwa kwa bidhaa za magendo ambazo pia hazina viwango kwa matumizi ya binadamu, Sukari hiyo na mafuta ya kula vimekamatwa kwenye bandari bubu za Mbweni jijini Dar es salaam.
3
Kama inavyoonekanamifuko ya sukari ya viwandani na mafuta ya kula vikiwa katika kituo cha polisi Mbweni Konondoni  jijini Dar es salaam.
4 5
Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Kipolisi ya Kawe ASP Dk.  Ezekiel Kyogo akiwaelezea waandishi wa habari jinsi oparesheni hiyo ilivyoendeshwa na kuwanasa watu hao.
6
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mh. Daniel Chongolo mkoani Dar es salaam na Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Kipolisi ya Kawe ASP Dk.  Ezekiel Kyogo wakionesha vifaa hivyo mbele ya waandishi wa habari.
7 8 9
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mh. Daniel Chongolo mkoani Dar es salaam na Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Kipolisi ya Kawe ASP Dk.  Ezekiel Kyogo wakiowaonyesha Ng’ombe wanaotumika kufaulisha magendo hayo.
10 11
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mh. Daniel Chongolo mkoani Dar es salaam na Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Kipolisi ya Kawe ASP Dk.  Ezekiel Kyogo wakiowaonyesha Ng’ombe wanaotumika kufaulisha magendo hayo.
12
Mmoja wa maaskari wa kituo cha Polisi Kawe akionyesha jinsi ng’ombe hao walivyo na uwezo wa kubeba mizigo na kasi kubwa  watembeapo kutoka eneo la bandari bubu hizo na kuelekea kwenye maghala yanayohifadhi magendo hayo.
13 14
Share To:

Post A Comment: