Mbunge wa Jimbo la Vwawa Mkoani Songwe ambaye pia ni waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga akizungumza kwenye mkutano uliofanyika katika Kijiji na Kata ya Nanyala katika ziara yake ya siku tano ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi iliyoanza jana tarehe 5 Machi 2019.(Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Sehemu ya wakazi wa Kijiji na Kata ya Nanyala wakifatilia mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Vwawa Mkoani Songwe ambaye pia ni waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga jana tarehe 5 Machi 2019.
Mbunge wa Jimbo la Vwawa Mkoani Songwe ambaye pia ni waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga akizungumza kwenye mkutano uliofanyika katika Kijiji na Kata ya Nanyala katika ziara yake ya siku tano ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi iliyoanza jana tarehe 5 Machi 2019.
Sehemu ya wakazi wa Kijiji na Kata ya Nanyala wakifatilia mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Vwawa Mkoani Songwe ambaye pia ni waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga jana tarehe 5 Machi 2019.
Na Mathias Canal, Songwe
Mbunge
wa Jimbo la Vwawa Mkoani Songwe ambaye pia ni waziri wa Kilimo Mhe
Japhet Hasunga jana tarehe 5 Machi 2019 ameanza ziara ya kukagua
utekelezaji wa miradi ya maendeleo sambamba na kusikiliza na kutatua
kero za wananchi.
Katika
ziara hiyo iliyoanzia katika Kijiji na Kata ya Nanyala Mhe Hasunga
amesisitiza ulazima wa mbolea kuwafikia wakulima kwa wakati kuanzia
msimu huu wa kilimo wa mwaka 2019/2020
“Katika
kipindi cha miaka kadhaa iliyopita Mbolea ilikuwa ikiishia Jijini Dar
es salaam badala ya kuwafikia wakulima jambo hilo tumelikataa ni lazima
mbolea ifike kwa wakulima kwa wakati” Alikaririwa na kuongeza kuwa
“Ni
jambo la kushangaza kuona mbolea nyingi inawekwa Dar es salaam wakati
hakuna uhitaji mkubwa wa mbolea sasa naagiza mbolea yote kuwafikia
wakulima ili kurahisisha huduma za kilimo”
Mhe
Hasunga pamoja na mambo mengine ameeleza kuwa Wizara ya Kilimo
imejipanga kuhakikisha kuwa masoko ya mazao mbalimbali yanapatikana ili
kurahisisha na kuongeza ufanisi wa kipato kwa wakulima.
Alisema
kuwa wakulima wamekuwa wakitumia nguvu nyingi katika kilimo lakini
masoko ya mazao yao yanakosekana na katika kulikabili hilo wizara
imeanzisha kitengo maalumu kitakachoshughulikia masoko.
Alisema katika kutekeleza hatua za utafutaji masoko Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli tarehe 4
Januari 2019 alishuhudia utiaji saini mkataba wa mauziano ya Tani
36,000 za mahindi kati ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA)
na Shirika la chakula Duniani (WFP).
“Kuna
Taasisi zangu zinazoshughulika na ununuzi wa mazao ya wakulima ambazo
ni Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) na Bodi ya nafaka na
Mazao mchanganyiko, tumezielekeza kuhakikisha zinanunua mazao mengi ya
wakulima kwa kufanya hivyo tutaimarisha soko la wakulima” Alisema
Katika
hatua nyingine Mhe Hasunga amewapongeza wakulima katika Jimbo la Vwawa
na Mkoa wa Songwe kwa ujumla wake kwa kujihusisha na kilimo kwa asilimia
kubwa huku akisisitiza ulazima wa kuongeza tija katika kilimo kwa
kutumia wataalamu mbalimbali.
Post A Comment: