Mwenyekiti wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Iringa Vijijini Juma Mapesa Makalah akimkabidhi fedha mmoja ya makepteini wa timu ambazo zilishiriki mashindano ya lukuvi cup ukanda wa Pawaga.
Katibu wa mbunge wa jimbo la Ismani Thom Malenga akiwa sambamba na diwani moja wa ukanda wa Pawaga wakati wa kuwa zawadi kwa washindi
Baadhi ya wachezaji walioshiriki Lukuvi cup mwaka 2018

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
 
Mbunge wa jimbo la Isman William Lukuvi amegawa zawadi za zaidi ya shilingi milioni arobain na moja kwenye mashindano ya William Lukuvi cup yaliyofanyika katika kata zote kumi na tatu katika jimbo hilo na kufanikiwa kuinua vipaji na kujenga afya kwa vijana walioshiriki mashindano hao.

Akizungumza wakati wa ugawaji wa vifaa hivyo katibu wa mbunge huyo Thom Malenga alisema kuwa wametumia zaidi ya shilingi milioni arobain na moja kwa ajili ya kununua vifaa pamoja na kutoa zawadi kwa washindi wa mashindano hayo kwa kila kata.

“Tumenunua mipira themenini (80) kila mpira shilingi elfu thelathini (30,000) na jezi tumenunua themenini (80) kila seti ya jezi inauzwa shilingi laki mbili na nusu (250,000) hapo kwa upande wa vifaa tu vya michezo ambavyo tuligawa kila kijiji ambacho kipo jimboni kwetu” alisema Malenga

Malenga aliongeza kuwa mashindano hayo yalikuwa yanafanyika kwa kila kata hivyo mshindi wa kwanza alijinyakulia kiasi cha shilingi laki saba (700,000), mshindi wa pili alijinyakulia kiasi cha shilingi laki tano (500,000) na mshindi wa tatu alijinyakulia kitita cha shilingi laki mbili na nusu (250,000),zawadi hizo zilitolewa kwa kila kata ya jimbo hilo.

“Utaona tumetumia zaidi ya shilingi million arobain na moja (41,250,000) kwa ajili ya vifaa na zawadi katika mashindano haya ya Lukuvi cup kwa mwaka huu tu na kila mwaka tumekuwa tukifanya mashindano haya kwa wananchi wetu wa jimbo letu la ismani” alisema Malenga

Aidha Malenga alisema kuwa mbunge wa jimbo hilo amekuwa na jitihada za makusudi za kusaidia timu za jimbo hilo kwenye mashindano mbalimbali kwa lengo la kukuza michezo kwa wapenda michezo wa jimbo hilo.

“Mimi naowaomba wanamichezo kinapofika kipindi cha mashindano hayo wajitokeze na kuonyesha vipaji vyao na kuweka sawa afya zao kwa kuwa sasa michezo ni ajira n analipa kweli kweli kama ukiangalia mpira wa miguuu sasa ndia ajira ambayo inaongoza kwa malipo kwa wachezaji hapa nchini” alisema Malenga

Kwa upande wake mwenyekiti wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Iringa Vijijini Juma Mapesa Makalah  alimpongeza mbunge wa jimbo hilo kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuleta maendeleo na kuinua na kuibua vipaji vya wachezaji kutoka jimbo hilo.

“Kwa dhati kabisa nampongeza mbunge huyu wa jimbo hili William Lukuvi kwa kazi kubwa anayoifanya kuleta maendeleo kwenye jimbo hili na kuinua michezo ni tofautia kwenye majimbo mengine ya wilaya hiyo ambako hawajawahi kuona hata michezo ikianzishwa na mbunge” alisema Makalah

Makalah aliongeza kwa kusema kuwa wanamichezo wa jimbo la Isman wanabahati kuwa ya kuwa na mbunge anayependa michezo huku akisema kuna jimbo la jirani tu wao kama viongozi hawajawahi hata kusikia mbunge wa jimbo hilo ajishughulisha kwenye michezo.

“Jamani vijana wenzangu waliulize majirani wezenu kama wamewahi kushiliki mashindano ya mbunge waulizeni msiogope lakini nyie wa jimbo hili la Lukuvi mnacheza mashindano haya kila mwaka na ndio faida ya kuwa na mbunge anayethamini vipaji vyenu” alisema Makalah

Lakini Makalah aliwaomba wananchi wa jimbo la Isman kuendelea kuwanga mkono chama cha mapinduzi kwa jithada ambazo zinafanywa na viongozi wao katika maeneo mbali mbali hapa nchi kwa lengo kuleta maendeleo na kuwa wazalendo na nchi yao.

“CCM bado inawapenda na itaendelea kuwapenda na kuwatumikia kwa kuwaletea maendeleo ya kila siku hivyo naomba kwa niaba ya viongozi wangu kuendelea kuichagua CCM kwenye chaguzi zote zinazokuja kwa ngazi zote na mtupe kula zote jamani ninaomba” alisema Makalah
Share To:

Post A Comment: