1
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP, Simon Sirro akiweka sahihi kwenye kitabu cha waombolezaji baada ya kuwasili nyumbani kwa marehemu Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi DCP Renatus Matanga Mbushi, aliyefariki dunia tarehe 03/03 mwaka huu huko Mkoani Mbeya alipokuwa kwenye ziara ya kikazi na mwili wake kusafirishwa kuja jijini Dar es Salaam kwa ajili ya taratibu za mazishi.(Picha na Jeshi la Polisi).
2
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP, Simon Sirro, akiteta jambo na Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu IGP Said Mwema wakati walipokutana nyumbani kwa Marehemu Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi DCP Renatus Matanga Mbushi, katika kambi ya Maafisa wa Polisi Oysterbay, Kinondoni jijini Dar es salaam, msiba huo ulitokea tarehe 03/03 mwaka huu huko Mkoani Mbeya alipokuwa kwenye ziara ya kikazi na mwili wake kusafirishwa kuja jijini Dar es Salaam kwa ajili ya taratibu za mazishi.(Picha na Jeshi la Polisi).
3
Maofisa wa Jeshi la Polisi wakiingiza mwili wa Marehemu Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi DCP Renatus Matanga Mbushi katika Kanisa la Parokia ya Mt. Petro lililopo Oysterbay  jijini Dar es salaam kwa ajili ya  misa ya kuuaga, msiba huo ulitokea tarehe 03/03 mwaka huu huko Mkoani Mbeya alipokuwa kwenye ziara ya kikazi na mwili wake kusafirishwa kuja jijini Dar es Salaam kwa ajili ya taratibu za mazishi.(Picha na Jeshi la Polisi).
4
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP, Simon Sirro akiaga mwili wa marehemu Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi DCP Renatus Matanga Mbushi, katika Kanisa la Parokia ya Mt. Petro Oysterbay jijini Dar es salaam msiba huo ulitokea tarehe 03/03 mwaka huu huko Mkoani Mbeya alipokuwa kwenye ziara ya kikazi na mwili wake kusafirishwa kuja jijini Dar es Salaam kwa ajili ya taratibu za mazishi.(Picha na Jeshi la Polisi).
Share To:

msumbanews

Post A Comment: