BENKI ya TIB Corporate waadhimisha wiki ya huduma kwa wateja kwa kuwatembelea wateja mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na MICHUZI BLOG leo Mkuu wa masoko na mahusiano wa benki ya TIB, Theresia Soka
  amesema kuwa lengo la kutembelea wateja wao ni kujitathimini jinsi wanavyotoa huduma kwa wateja mbalimbali wa benki hiyo katika wiki ya huduma kwa wateja.

"Benki ya TIB Corporate katika maadhimisho ya wiki ya huduma kwa mteja tunawatembelea wateja wetu ili kujitathimini ni wapi tunakosea ili tufanye marekebisho."

Pia amewakaribisha wateja mbalimbali kujiunga na benki hiyo kwani benki hiyo 
 
Nae Mkurugenzi wa Fedha Mamlaka ya Usimamiz wa Bandari (TPA), Nuru Mhando amewashukuru wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate kwa kuchagua kumtembelea na anajivunia kuwa mteja wa benki hiyo.

Mkurugenzi wa ukaguzi wa ndani wa benki ya TIB Corporate, Edwin Katanga akimkabidhi ua Mkurugenzi wa Fedha Mamlaka ya Usimamiz wa Bandari (TPA), Nuru Mhando mara baada ya kumtembelea ikiwa ni kuthamini mchango wa taasisi mbalimbali katika wiki ya huduma kwa wateja.
Mkurugenzi wa Fedha Mamlaka ya Usimamiz wa Bandari (TPA), Nuru Mhando kulia akizungumza na wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate mara baada ya kutembelewa na wafanyakazi hao ikiwa ni kuadhimisha wiki ya huduma kwa mteja.
Wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Fedha Mamlaka ya Usimamiz wa Bandari (TPA), Nuru Mhando mara baada ya kutembelea ofisi ya TPA kwaajili ya kuadhimisha siku ya huduma kwa mteja ambayo hufanyika kila Oktoba.
Mkuu wa masoko na mahusiano wa Benki ya TIB, Theresia Soka akizungumza na Michuzi Blog kuhusiana na wiki ya huduma kwa mteja ambayo hufanyika kila mwaka ifikapo Oktoba katika taasisi mbalimbali na mashirika mbalimbali duniani kote.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: