Mamia ya watu wanahofiwa kufariki baada ya kivuko cha MV Nyerere walichokuwa wanasafiria kuzama katika ziwa Viktoria mkoani Mwanza magharibi mwa Tanzania.

Wizara ya uchukuzi na mawasiliano Tanzania TEMESA imetoa taarifa ikithibitisha mkasa huo kilichotokea kati ya Ukara na Bugolora wilayani Ukerewe majira ya mchana.

Maafisa wa serikali nchini wamethibitisha kwamba shughuli ya kuwaokoa manusura inaendelea.

Taarifa za awali zinaeleza kwamba kivukio hicho kilikuwa kimebeba mamia ya abiria.

Kamishna wa eneo jirani la Mara, Adam Malima ameeleza kwamba maafisa kadhaa kutoka enoe hilo wakiwemo polisi na jehsi la majini wanaelekea kujiung akatika jitihada za uokozi.

''Hatuijui hali halisi tunakwenda kuikagua kwanza alafu baadaye tutatoa tamko rasmi.

Malima ameeleza kwamba maboti ya polisi na jeshi watashirikaian akatika zoezi hilo la uokozi.

''Tunaomba mungu atupe subira kwa wakati huu, na tusishuhudie idadi kubwa ya vifo

Mkasa huo umewashutusha wengi nchini kama mwanamke mmoja aliyeshuhudia mkasa huo ambaye alionekana kujawa na hisia.

''Tazama Tazama.. Kivuko kile pale kimezama …….miili inaelea, imezama sasa hivi''.Umati mkubwa wa watu umeshuka ufukweni kutazama jitihada za uokozi

Share To:

Anonymous

Post A Comment: