Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Benki ya  CBA  imetoa msaada wa shilingi milioni 4 kwa shule ya msingi Singisi kwa ajili ya mabati pamoja na ukarabati wa shule hiyo ili kusaidia kutatua changamoto ya uhaba wa madarasa na uchakavu wa majengo.

Mkuu wa Idara ya wateja ,masoko na mawasiliano,Julius Konyani  alisema kuwa wameamua kutoa msaada huo ili kusaidia  watoto wa kitanzania waweze kupata elimu bora ambayo itawasaidia kujikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini.

Julius alisema kuwa benki hiyo imeamua kurudisha sehemu ya faida kwa wananchi kwa kutoa fedha hizo licha ya msaada huo wamekua wakisaidia chumba cha watoto njiti kwa kutoa vifaa vya kitaalamu ili kuokoa maisha ya watoto.

Mkuu wa Shule hiyo Safira Ndelwa    ameshukuru msaada huo ambapo amesema kuwa msaada huo utawasaidia kumalizia ujenzi wa uzio wa shule hiyo pamoja na kukarabati majengo ya shule hiyo ambayo ni chakavu.

Hata hivyo ameiomba benki hiyo iweze kuwasaidia kuwajengea vyumba vya madarasa kwani shule hiyo inakabiliwa na uhaba wa madarasa hali inayosababisha msongamano darasani inayowalazimu kuingia darasani kwa awamu huku walimu wakifundisha kwa zamu.

“Tunaomba benki ya CBA isituache iendelee kutusaidia katika maeneo mengine ambayo kuna changamoto ili wanafunzi waweze kusoma katika hali bora” Alisema Ndelwa

Diwani wa Kata ya Seela Singisi Penzila Palangyo amesema kuwa ushiriki wa sekta binafsi katika maendeleo ya elimu ni muhimu ili kuhakikisha kuwa sekta ya elimu inasonga mbele na kusaidia maisha ya watu wengi
Share To:

msumbanews

Post A Comment: