" LOLIONDO" yarudi tena! Pengine hii inaweza kuwa stori nyingine ya kuvutia kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, baada ya mtu mwingine kujitokeza na kuanza kutoa huduma inayofanana na ya Babu wa Loliondo.

Mganga huyo wa kienyeji ametambulika kwa jina moja la Yakub amekua akifanya huduma hiyo maeneo ya Feri ambapo amejipambanua kutibu magonjwa mbalimbali kwa kutumia dawa anayoweka kwenye chupa ya maji ya kunywa.

Tayari kundi kubwa la watu limeanza kujitokeza kwa Babu huyo ambaye tofauti yake na yule wa Loliondo huyu wa Dar amekuwa akichaji Shilingi 3,000 kama gharama ya dawa zake.

Watu kadhaa ambao wameshatumia dawa za Babu huyo wamekiri kuona mabadiliko ambapo wamemsifu kwa kuwa na dawa ambazo zinatibu kwa haraka.
Share To:

Post A Comment: