Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof.  Joyce Ndalichako ameigiza Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi(VETA)  kuhakikisha inapeleka fedha kwa wakati katika ofisi za Kanda na Vyuo vya  Wilaya na Mikoa ilikuharakisha utekelezaji wa mipango mbalimbali ya Mamlaka hizo.

Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo akiwa ziarani mkoani Katavi    ambapo amesema VETA kanda, Mikoa na Wilaya zimekuwa na changamoto za kujiendesha kutokana na kutokuwa na fedha za kutosha.

 Amesema amesikitishwa kuona baadhi ya mitambo katika Chuo cha VETA Mpanda iliyonunuliwa kwa gharama kubwa na Serkali haifanya kazi kwa kukosekana fedha kidogo za ufungaji wa mitambo hiyo katika karakana za chuo hicho .

“Ukiangalia VETA za mikoani na wilayani zinahitaji fedhak kidogo tu ili zipige hatua lakini hazitolewi, naagiza VETA Makao Makuu kuhakikisha katika mipango yenu mhakikishe mnaweka usawa wa upelekaji fedha kwa VETA zote nchini ili nazo ziweze kupiga hatua katika kutoa mafunzo,”amesema Waziri Ndalichako.

Katika hatua nyingine Waziri Ndalichako ameahidi kutoa cherehani mbili kwa wanafunzi Gift Giles na Benitha William wwenye umri wa miaka kumi na tano ambao wamejiunga katika Chuo cha VETA Mpanda baada ya kutokuchaguliwa kuendeleana masomo ya kidato cha kwanza.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Katavi Amos Makala amenuahidi Waziri kuwa atakisimamia Chuo cha VETA Mpanda ili kiweze kuwa na tija kwa wanakatavi.



Imetolewa na:
Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
16/8/2018
Share To:

msumbanews

Post A Comment: