Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mheshimiwa William Ole Nasha ametembele Chuo Cha Ualimu Nachingwea na kuridhishwa na kiwango cha ukarabati kinachoendelea ambapo kiasi  cha shilingi bilioni 1.3  kimetolewa kwa ajili ya ukarabati huo.

Akizungumza na watumishi katika Chuo hicho Naibu Waziri Ole Nasha amepongeza Kiwango Cha ufaulu kwa wanafunzi wa kidato Cha sita kwa mwaka 2018 kwa mkoa wa Lindi kushika nafasi ya pili Kitaifa.

Naibu Waziri pia amewataka walimu kuhakikisha wanasimamia, wanahamasisha na kuelimisha jamii kuachana na na mila na desturi potofu zinazochangia watoto kuacha shule ikiwa ni pamoja na kushiriki katika unyago.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Ole Nasha ametembelea  na kuipongeza Halmashauri kwa kuwa na wazo la kuwa na Shule ya Sekondari ya wasichana Nachingwea na kuwa hiyo itasaidia watoto  wa kike kuondokana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na wanafunzi kutembea umbali mrefu.

Mheshimiwa Ole Nasha amesema Wazazi na wadau wana wajibu wa kuwalinda watoto wa kike dhidi ya vitendo vinavyowanyima fursa, ambapo amewataka Walimu kuhakikisha wanasimamia  wanafunzi ili waweze kufikia malengo yao.  itachukua hatua kwa wazembe.

Naibu Waziri ameahidi kusaidia ujenzi  wa vyumba vya madarasa viwili na nyumba 2 za walimu ili kupunguza changamoto za shule hiyo.

Imetolewa na:
Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
17/8/2018
Share To:

msumbanews

Post A Comment: