Hospitali zote nchini pamoja na vituo vyote vya kutolea huduma za Afya zimepigwa marufuku kuonesha miziki katika maeneo yakutolea huduma na badala yake kutakiwa kuweka jumbe zinazohusu Elimu ya Afya kwa umma pindi wanapongoja kupata huduma.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile hapo jana wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika ukumbi wa halmashauri ya Muleba katika Mkoa wa Kagera.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: