Jaji Salma Maghimbi aliyesikiliza kesi ya mauaji ya bilionea Erasto Msuya na kuwahukumu adhabu ya kifo washitakiwa watano, ametishiwa kuuawa na mtu asiyejulikana

Inadaiwa mtu huyo alipiga simu kupitia simu ya mezani(ofisini) na kumtisha kummiminia risasi kama za bilionea Msuya kwa kitendo cha kumhukumu ndugu yake kunyongwa

Mtu huyo alimwambia Jaji kuwa iwapo watashindwa kumuua nyumbani au barabarani, basi wangetekeleza mauaji hayo akiwa katika eneo la mahakama Kuu

Kutokana na vitisho hivyo, Jeshi la Polisi limemuongezea ulinzi Jaji huyo ambaye sasa amehamishiwa divisheni ya Ardhi jijini Dar lakini bado anamalizia kesi zake jijini humo

Msuya aliuawa kwa kupigwa risasi na bunduki ya kivita aina ya SMG Agosti 7, 2013 eneo la Mijohoroni wilayani Hai mkoani Kilimanjaro
Share To:

msumbanews

Post A Comment: