Kampuni ya simu na kompyuta Apple imekuwa ni kampuni ya umma ya kwanza duniani kuwa na thamani ya dola trilioni moja $1 trillion.
Bwana Jobs, ambae alifariki dunia mwaka 2011 na kurithiwa na Mkurugenzi Mkuu Tim Cook, alisimamia maendeleo ya iPhone, ambayo ilibadili kabisa kipato cha Apple.
Thamani ya soko la watengezaji wa iPhone imefikia kiwango hicho mjini in New York Alhamisi na hisa zake zilifikia rekodi mpya ya $207.39.
Hisa zake zimekuwa zikipanda tangu Jumanne wakati kampuni hiyo iliporipoti kupata matokeo mazuri kuliko ilivyotarajiwa katika kipindi cha miezi mitatu kuelekea mwezi Juni.
Apple iliipiku kampuni shindani za Silicon Valley kama vile Amazon na Microsoft na kuweza kufikia hadi thamani ya dola trilioni $1.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: