Msafara wa Waziri wa Maliasili, Dkt. Hamisi Kigwangalla umesimamishwa na kundi kubwa la wananchi wa kijiji cha Kisumba kilichopo wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa wakiwa na mabango yanayoeleza kero zao mbalimbali.

Miongoni mwa kero hizo ni pamoja na wanyamapori jamii ya Tembo kuvamia mashamba yao na hivyo kukosa chakula na kukosekana kwa huduma muhimu ya maji iliyotokana na kuchakachuliwa kwa mradi wa maji wa jumla ya shilingi milioni 663 kijijini hapo.

Mkazi wa kijiji hicho, Leonard Kiombe amesema mara nyingi wamekuwa wakiwasimamisha viongozi kwa sababu ya kero ya maji, "tulipata mradi wa milioni 663 wakasema zaidi ya vijiji 6 vitapata maji lakini kijii cha kisumba mpaka sasa hatuna maji, mradi umechakachuliwa na maji hayatoki".

Akijibu kero hizo, Waziri Kigwangalla amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii kuhakikisha Taasisi za Uhifadhi wa Wanyamapori pamoja na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS wanashirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kutengeneza vikundi vya wananchi wa vijiji vyote vinavyopakana na Hifadhi ya Msitu wa Kalambo na Pori la Akiba Lwafi ili wawezeshwe fedha za mikopo ama mizinga ya kufugia nyuki ambayo wataipanga pembezoni mwa mashamba yao ili kuzuia tembo wasiingie kwenye mashamba.

"Teknolojia hiyo imethibitika kusaidia kudhibiti tembo walilete madhara kwenye makazi ya watu kwa kuwa nyuki hufukuza tembo na endapo tembo nao wakinusa harufu ya nyuki huwa sio rahisi kusogelea maeneo hayo, hivyo ameagiza mradi huo utekelezwe ndani ya kipindi cha miezi miwili kabla mvua za masika kuanza", amesisitiza Kigwangalla.

Waziri Kigwangalla pia ametoa wito kwa wananchi hao kuacha kufanya shughuli zao kwenye maeneo ya hifadhi ikiwemo maeneo ya mapito ya wanyamapori kwa kuwa kufanya hivyo ni kuhatarisha maisha na ustawi wao
Share To:

msumbanews

Post A Comment: