Viongozi wote wa Chadema Kata ya Muungano, wakiongozwa na Godliving Emmanuel Kimaro ( Baba Diana) Mwenyekiti wa Kata ya Muungano na Ibrahimu Hamis Mkindi (Mparee) Mwenezi wa Chadema Kata Muungano kutoka Wilaya ya Hai wamejivua uanachama wa Chadema na kujiunga na CCM.

Viongozi hao wamepokelewa na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Taifa Kamaradi Humphrey Polepole kwenye Mkutano wa hadhara Moshi Mjini Kata ya Mawenzi wakati akimnadi Mgombea wa Udiwani wa CCM Kata ya Mawenzi Ndg. Apaikunda Ayo Naburi.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: