Watu zaidi ya 20 wa kaya sita katika Mtaa wa Nyakabungo wilayani Nyamagana mkoani Mwanza hawana mahali pa kuishi baada ya kikundi cha wakazi wa mtaa huo kudaiwa kuvamia na kuzichoma moto nyumba tano kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kisasi kufuatia baadhi ya familia hizo kuhusishwa na matukio ya wizi.

Tukio hilo lililotokea majira ya saa nane za usiku wa kuamkia Julai 25 mwaka huu ambapo kikundi hicho cha watu waliokuwa na silaha za jadi kilivamia nyumba hizo na kuamrisha watu kutoka nje ya nyumba zao kabla ya kuharibu mali na samani za ndani na baadaye kuzichoma moto nyumba hizo 

Tazama fulu video hapo chini
Share To:

msumbanews

Post A Comment: