Mwanasiasa Mkongwe na aliyewahi kuwa Katibu MKuu wa chama cha CCM,Ndugu Yusuf Makamba akimtambulisha na kumnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Buyungu Mh.Christopher Chiza wakati wa uzinduzi wa Kampeni za ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo wilayani Kakonko mkoani Kigoma 
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi akiwa ameambatana na mgombea Ubunge wa jimbo la Buyungu Mh.Christopher Chiza wakati wa uzinduzi wa Kampeni za ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo wilayani Kakonko mkoani Kigoma.
Mwanasiasa Mkongwe na aliyewahi kuwa Katibu MKuu wa chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu Yusuf Makamba  akiwa katika picha ya pamoja na baaadhi ya Wabunge wa chama hicho mapema jana wakati wa uzinduzi wa Kampeni za ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Buyungu wilayani Kakonko mkoani Kigoma,Pichani kulia ni Mh Bashe,Peter Serukamba na mwisho kabisa kushoto ni Mh Nape.
Baadhi ya viongozi na Wabunge wa CCM wakifurahia shuughuli za uzinduzi wa kampeni za Ubunge ndani ya jimo hilo la Buyungu wilani Kakonko mkoani Kigoma 
Baadhi ya Wanachama na Wafuasi wa chama cha Mapinduzi (CCM),wakiwa wamebeba mabango yenye jumbe mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Kampeni za ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Buyungu wilayani humo 
Na Rhoda Ezekiel Kigoma

KATIBU MKUU wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Taifa Bashiru Ally amewaapisha wanachama wapya 269 kutoka vyama vya upinzani akiwemo aliekuwa Mbunge wa jimbo la Kasulu Vijijini Agripina Buyogera na Mwenyekiti wa Chama cha NSSR Mkoa na Wilaya ya Kasulu Hitra Joseph Gelvasi Bahenga katika amkutano wa kampeni za uchaguzi Wilayani Kakonko mkoani Kigoma.

Tukio hilo lilifanyika jana Katika mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Buyungu wilayani humo wakati akimnadi mgombea wa Chama hicho ambapo wananchi hao walioamua kujiunga na CCM na kuwaomba wananchi kuendelea kukiamini na kumpa kura mgombea wao.

Amesema wanachama hao hawajawanunua ila wamevutiwa na utekelezwaji wa Ilani ya Chama na amewaahidi wananchi kabla ya uchaguzi huo kuisha watapokea vigogo wengi na watawapokea hawata wabagua wote watakaotaka kujiunga na CCM na wote wanahaki ya kujiunga.

" Milango ya wanachama wapya iko wazi na tuna wakaribisha sana na hawa ndio wamefungua mlango tunawakaribisha wote CCM haina mwenyewe wote tuna sifa ya kuwa wanachama.Sasa tunapokea wote na hatuko tayari kununua Watu kutoka vyama vingine wataona mambo wenyewe watakuja," alieleza Bashiru.

Akimkaribisha mgeni rasmi katika uzinduzi wa kampeni hizo Ally alisema CCM ni chama cha wanyonge kipo kwaajili ya kuwatetea katika kuleta maendeleo hivyo amewaomba Wanakakoko kumchagua Chiza ili akafanye kazi na Chama cha Mapinduzi.Alisema anatambua mchango wa Chiza kwa wanakakonko na yapo mengi ambayo ameyafanya kwa Jimbo la Buyungu suala la kuwashawishi wananchi wasimchague kwa kigezo kwamba ni mzee hii sio kweli wamuamini wampe kura aweze kuwaletea maendeleo zaidi.

"Tunae mgombea ambae tunamnadi kwa sifa zake angalia elimu yake busara zake mchango wake katika jamii kupitia mkutano huu wana CCM wote watakao hisika na kampeni muwe na moyo wa kuvumilia mkitupiwa matusi msirudishe matusi hayo CCM ni chama cha wastaarabu muwe wavumilivu" alisema Katibu Mkuu.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: