Msanii Belle 9 amesema moja ya wasanii asiyowaelewa katika Bongo Flava ni Madee.

Muimbaji huyo akipiga stori na JJ wa Jembe FM amesema kuwa kutokana anasikiliza wachanaji wengi wanaofanya vizuri anahisi kuna kitu anakikosa kutoka kwa Madee.
“Honesty, let me be honesty, Madee huwa simuelewi. I don’t know, ujue kuna wasanii inafika kipindi unasikiliza unasema huyo mtu ana-release beat sio wimbo tena,” amesema.
“Labda kwa vile nasikiliza rappers ambao wanajua sana au kuna kitu nakitegemea kutoka kwake kutokana muda mrefu yupo kwenye game, kuna kitu nakimisi, so naona kama nikimsiliza na lose,” amesisiza.
Belle 9 ambaye anafanya vizuri na ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la Dada, ameongeza kuwa mara nyingi ni vigumu mtu anayetoa kauli kama yake kueleweka ila yeye amesema kile ambacho anaona kipo sawa na kuwataka mashabiki wa Madee kuchukulia kawaida.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: