Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Mashaka Gambo,  leo amewaongoza maelfu ya wananchi mkoani hapa kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) ambayo Kimkoa shamra zake zilifanyika katika Uwanja wa Sheik Amri Abeid.

Wafanyakazi wa serikali na makampuni mbalimbali binafsi walijumuika pamoja kusherehekea siku hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo (wa tatu kushoto) akiwa amefuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Mh: Fabian Daqarro pamoja Katibu Tawala wa Mkoa Richard Twitega  na viongozi wa wafanyakazi serikali, mashirika ya umma na taasisi binafsi Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.
Moja ya vikosi vya makampuni ya ulinzi Intellegence Security vikijiandaa kuingia uwanja wa Amri Abeid kwa maandamano ya Siku ya Wafanyakazi.


 Baadhi ya wafanyakazi wakicheza kwa furaha wakijiandaa kuingia uwanjani.

Baadhi  ya makundi yaliyokuwa yakijiandaa kuingia uwanjani kuadhimisha siku ya Mei Mosi

Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Application yetu ya Msumba News ili upate habari zetu kwa wepesi zaidi kama vile Magazeti kuliko ilivyo sasa.

Tumekurahisishia; 
Share To:

msumbanews

Post A Comment: