Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amemwagiza katibu tawala mkoa wa Arusha Richard Kwitega kuwachukulia hatua za kinidhamu na kiutumishi watumishi sita (6) wa halmashauri ya wilaya ya Longido kutokana na makosa mbalimbali ya kiutumishi.
Miongoni mwa watakaochukuliwa hatua ni pamoja na aliyekua Kaimu Afisa Utumishi wa wilaya hiyo kwa mwaka 2016/17 Bwana Steven Mbombe na msimamizi wa mfumo wa mishahara LGHRIS Bwana Derek Rutenge kwa uzembe wa kuwalipa mishahara watumishi wawili marehemu na kuisababishia hasara serikali ya shilingi milioni saba na elfu themanini na nane (7,088,000/=).
Katika taarifa ya CAG kwa mwaka wa fedha 2016/17 halmashauri ya Longido imepata hati inayotia mashaka.
Post A Comment: