Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma Kasheku, amefungukia madai yaliyowahi kutolewa na Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe, kwamba walitekwa na watu wa usalama wa Taifa ni ya uongo na kwamba kilichotokea walikamatwa na askari na mbinu zilizotumika ni zile wanazofundishwa bungeni.

Musukuma ametoa kauli hiyo jana  wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha Kikaangoni kinachorushwa na  EATV , ambapo alifafanua kwamba walikuwa wakidhaniwa kufanya uhalifu.

Musukuma alisema kwamba "Mara ya kwanza kulala polisi nimelala nikiwa mwana- CCM, mara ya kwanza Dodoma, mara ya pili ni Geita, na nilikubali kwa sababu wala hatukutekwa, nilikuwa na kina Bashe, nilimsikia rafiki yangu Hussein Bashe alisema tumetekwa, hatukutekwa".

"Tulikamatwa tukapelekwa polisi, tukapekuliwa, tulipoonekana hatuna hatia tukaachiwa , hatukutekwa. Sikumjibu Hussein Bashe aliposema tumetekwa kwa sababu sikuwepo, nasema hapa hatukutekwa," Musukuma.

Aprili 11, 2017 Mbunge wa Nzega Mjini(CCM) Hussein Bashe aliwataka wabunge kuacha unafiki kuhusu Usalama kuwateka watu na kwamba yeye ni mmoja wa watu waliokamatwa wakati wa mkutano Mkuu wa CCM.

"Mimi nimekamatwa na kuteswa na Usalama wa Taifa. Nimenyanyaswa sana nchi hii. Ikibidi mnifukuze CCM - " alisema Bashe wakati Waziri wa Tamisemi,(kabla hajaenguliwa katika nafasi hiyo) George Simbachawene kumtaka Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuthibitisha kuwa matukio ya ukamataji yanafanywa na usalama wa Taifa.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: