Kocha wa zamani wa Yanga, George Lwandamina, rasmi ametambulishwa na uongozi wa Zesco United ya Zambia kuwa Mwalimu Mkuu wa timu hiyo.

Lwandamina alirejea nchini kwao kimyakimya akiiacha Yanga kutokana na madai ya fedha za mishahara ambazo hajalipwa.

==>> Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>

Zesco wameamua kumrejesha tena Lwandamina wakiwa na imani kuwa atakisaidia kikosi hicho kufanya vizuri katika mashindano ya ligi na kimataifa.

Lwandamina ametambulishwa jana wakati Yanga ikiwa tayari imeshaanza kazi na Mkongomani mpya, Mwinyi Zahera aliyekuja nchini hivi karibuni kuchukua mikoba yake
Share To:

msumbanews

Post A Comment: