Aliyewahi kugombea ubunge katika Wilaya ya Tarime kupitia chama cha ACT wazalendo ameamua kukihama chama hicho kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kuunga mkono serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania chini ya Mh John pombe magufuli.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa CCM Wilayani tarime aliyekuwa mgombea wa ubunge wilayani hapo kupitia ACT Wazalendo Tarime mjini 2015 Deogratias Meck amesema kuwa ameamua kuhamia CCM kwa kile alichotaja kuwa ni kukubali kazi inayofanywa na serikali ya chama hicho.
Akipokelewa na mwenyekiti wa chama hicho wilaya Mh Daudi Ngicho amesema kuwa sasa Tarime ni muda muafaka kwa wanatarime kutambua mazuri yanayofanywa na chama hicho nakukiuunga mkono kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kupata maendeleo ndani ya wilaya na Mkoa wa Mara kiujumla.
Pia Ngicho amewaasa wanachama wapya waliohamia katika chama hicho kuwa wazalendo na nchi yao nakutorubuniwa na wachache wasioitakia mema nchi yao.
Wanachama waliohamia chama cha mapinduzi wametajwa kuwa ni Joseph Antony mkurugenzi wa Mipango na uchaguzi CUF wilaya ya Tarime ,Angelina Joseph KATIBU wa Kata sabasaba ACT ,Abigael Chacha,Deborah Chacha,Agnes Japhet , Ibraham Juma Sengamgoda KATIBU ACT wilaya Tarime ,Deogratias Meck mwanachama na mgombea ubunge kupitia ACT wazalendo 2015 Tarime.
Post A Comment: