Mbunge wa Kawe (Chadema),  Halima Mdee ameitaka Serikali kuwa na huruma na watumishi wake iliowaondoa kazini baada ya kubainika kuwa na vyeti feki.

Mdee ametoa kauli hiyo bungeni mjini Dodoma leo Jumatano Mei 23, 2018 wakati akiuliza swali la nyongeza, kubainisha kuwa  kuna watumishi waliotumia vyeti vya watu wengine kujiendeleza kielimu na wamefanya kazi kwa uadilifu mkubwa.

Hata hivyo, Waziri wa Nishati, Angellah Kairuki ambaye wakati wa uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma ukianza alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora) amesema hakuna malipo wala huruma yoyote itakayotolewa kwa wafanyakazi hao.

" Mdee mdogo wangu na dada yangu wewe ni mwanasheria lazima ujue kuwa hakuna kitu kama hicho kwa hiyo Serikali haiwezi kuwalipa au kuwapa msamaha," amesema Kairuki.

Amesema kwa kuzingatia maelezo hayo, mjadala huo utakuwa umefungwa kwani waliostahili kurudi kazini walisharudishwa.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: