Wiki Kadhaa baada ya Video yao ya uchi kusambaa mitandaoni, Bill Nass amefunguka kuwa tayari kuna kuna ngoma ameshafanya na Nandy muda ukifika wataachia.

Hit maker huyo wa Tagi Ubavu amesema hayo katika kipindi cha Kikaangoni cha EATV na kuongeza kuwa mrembo huyo ni rafiki yake tu kwa sasa.

“Kuna wimbo tumefanya pamoja, wimbo umefanywa chini ya S2kizzy hivyo naamini muda ukifika utatoka tu ila nachojua ni wimbo mkali, kuhusu jambo ambalo limetokea,” amesema Bill.

Rapper huyo ameongeza, “Kuhusu mimi na yeye tayari nilishaomba radhi kwa wananchi na sasa maisha ya kawaida yanaendelea, hivyo hatuna tofauti yoyote ile kwa kuwa yule ni rafiki yangu na nina iheshimu sana familia yake akiwa pamoja na mama yake kwa kuwa ni mtu ambaye amekuwa akijitoa sana kusupport kazi za mwanae.”
Share To:

msumbanews

Post A Comment: